About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, October 7, 2011

NI NGUMU KUAMINI,LAKINI ASHIKILIWA NA POLISI KWA KUSABABISHA KIFO AKILAZIMISHA PENZI

Na Mwandishi Wetu, Songea
JESHI la Polisi Mkoani Ruvuma limemtia mbaroni Elly Millinga (33) Mkazi wa Kijiji cha Matiri Wilayani Mbinga kwa tuhuma za kumchoma kisu sehemu za tumboni Mzazi mwenzake Florida Mhaiki (26) Mkazi wa mtaa  wa Masumuni Mbinga mjini ambaye anadaiwa alikataa kufanya nae mapenzi
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Naftan Mantamba alisema kuwa tukio hilo lilitokea Octoba 7 mwaka huu majira ya saa 6.30 huko katika Mtaa wa Masumuni Mbinga mjini.
Mantamba alifafanua kuwa siku hiyo ya tukio Florida alichomwa kisu sehemu za tumboni na mzazi mwenzake Millinga ambaye alifika nyumbani kwa Florida majira ya saa za jioni ya Octoba 6 mwaka huu na kuanza kuongea nae kwa lengo la kumshawishi mzazi mwenzake waendelee kuishi kama mke na mume
Ameeleza zaidi kuwa Millinga pamoja na kutoa ushawishi huo Florida alikataa katakata na kudai kuwa watoto wawili aliozaa nae ameshindwa kuwahudumia hivyo hakuna sababu yeyote ya msingi ya kuridhia kurudiana na Millinga.
Amesema kuwa ilipofika majira ya saa 3 usiku ya Octoba 6 mwaka huu usiku Florida alimweleza mzazi mwenzake Millinga kuwa muda wa kwenda kulala umefika hivyo aliamua kumpatia nafasi ya kulala chumba ambacho kipo uani mwa nyumba kubwa na Millinga alienda kulala.
Amefafanua zaidi kuwa ilipofika saa 6 usiku Millinga aliamka na kwenda hadi kwenye chumba ambako Florida alikuwa amelala na kumtaka amfungulie mlango na baada ya kuingia aliendelea kumsihi Florida ili akubaliane na ombi alilomweleza hapo awali lakini ombi hilo halikuweza kukubalika ndipo Millinga alipoamua kuchukua kisu mfukoni na kumchoma sehemu za tumboni.
Ameeleza zaidi kuwa Florida baada ya kuchomwa kisu na mzazi mwenzake alipiga kelele kwa lengo la kupata msaada majirani walifika kwenye eneo la tukio na kumkuta Florida akiwa kwenye hali mbaya na kwenye chumba chake kulikuwa kumetapakaa damu.
Amesema kuwa majirani walimchukua Florida na kumkimbiza kwenye hospitali ya Serikali ya Mbinga kwa matibabu ambako alifari dunia wakati akiwa anaendelea kupata matibabu na polisi baada ya kupata taarifa ya tukio hilo walikwenda kwenye eneo la tukio na walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa Millinga ambaye kwasasa anaendelea kuhojiwa kuhusiana na tukio hilo.
MWISHO

No comments:

Post a Comment