About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, October 6, 2011

ANYWA SUMU,AFARIKI BAADA YA KUONYWA KUACHA UASHERATI MBAMBABAY

Na Mwandishi Wetu,Songea
JANETH Mwanjali ni msichana mwenye umri wa miaka 15 mkazi wa mji mdogo wa Mbamba bay uliopo Wilayani Nyasa Mkoa wa Ruvuma amefariki dunia baada ya kunywa dawa ya kuulia panya iliyokuwa imehifadhiwa nyumbani kwa wazazi wake.
Akizungumza na mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/  Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Naftani Mantamba amesema kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 4 asubuhi nyumbani kwa wazazi wa Janeth.
Mantamba amesema kuwa siku hiyo kabla ya tukio kutokea  inadaiwa kuwa Janeth aliitwa na mama yake mzazi Anna Kalima ambaye alikuwa akimuonya aache tabia ya kulala kwa wanaume na baadaye ulitokea ugomvi kati yake na mama yake ambaye alikuwa akimtuhumu kuwa anamuonea wivu kisha alikwenda ndani ya nyumba na kutafuta dawa ya kuulia panya ambayo aliinywa.
Amesema kuwa baada ya kuinywa dawa hiyo muda mfupi alianza kubadilika na hali yake ikawa mbaya hivyo mama yake mzazi aliamua kumchukua na kumpeleka hadi Kituo cha afya cha Mbamba bay ambako muda mfupi baadaye alifariki dunia akiendelea kupatiwa matibabu.
Mantamba amesema kuwa Chanzo cha tukio hilo ni kwamba Janeth alikuwa amegombana na mama yake mzazi aliyekuwa akimkanya kuwa aache tabia ya kulala nje kwa wanaume jambo ambalo lilimtia hasirĂ¡ na kuchukua uamuzi wa kutafuta dawa ya kuulia panya na kunywa kwa lengo la kujiua.
Hata hivyo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Mantamba ameeleza kuwa kwasasa Polisi wanaendelea kufanya upelelezi wa kina kuhusiana na tukio hilo licha ya kuwa Upelelezi wa awali umebaini kuwa Janeth alipandwa na hasira wakati anaonywa na mama yake mzazi.

1 comment:

  1. siku zake zilifika alikuwa ameshaitwa.du dunia na maisha yalivyo matamu! amewaachia wengine!?.

    ReplyDelete