About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, October 2, 2011

KAMATI YA MAADILI YA CCM MKOA WA RUVUMA YAWAHOJI MADIWANI WATANO KUHUSU SAKATA LA UMEYA

Na, Mwandishi Wetu,Songea

KAMATI ya Maadili ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma imewahoji Madiwani watano wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea ambao walituhumiwa na Chama hicho Wilaya ya Songea mjini kuwa wamekisaliti chama kwa kumpigia kura za hapana mgombea Umeya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

Kamati hiyo iliyokuwa na wajumbe Corneus Msuya ambaye ni Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoa wa Ruvuma,Emmanuel Mteming'ombe ambaye ni Katibu wa CCM mkoa wa Ruvuma,Henriet Ndimbo ambaye ni Katibu wa Uchumi na Fedha wa chama hicho mkoa, na Mama Litunu iliwahoji Madiwani hao ili kujiridhisha na tuhumu walizotuhumiwa nazo na CCM Wilaya ya Songea Mjini

Madiwani ambao wamehojiwa ni Christian Matembo(SeedFarm) Victor Ngongi(Ruvuma)Kurabest Mgwasa(Msamala) Faustine Mhagama(Mshangano) na Genfrida Haule diwani wa Viti Maalum wa chama hicho

Kwa mujibu wa Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma Emmanuel Mteming'ombe akizungumza na mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ alisema kuwa kikao hicho cha Maadili kilikuwa kinawapa fursa ya kujitete madiwani walihotuhumiwa

Mteming'ombe alieleza kuwa kimewahoji madiwani hao na chama kimetafakari tuhuma zao na majibu ambayo wamejitetea,baada ya hapo kitatoa onyo kwa madiwani wote akiwemo na Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Emmanuel Nchimbi kutokana na utomvu wa nidhamu aliouonyesha katika uchaguzi huo wa Umeya wa Songea mjini

Mtandao huu utaendelea kuwajuza wasomaji wake kila kitu kitakachojili bila kumuonea mtu,kumuogopa kwa wadhifa wake ili kuwawezesha wadau wa mtandao huu kujiridhisha na kutafakari viongozi wao waliopewa dhamana na wananchi walivyokuwa na tabia ya uroho wa madaraka kwa faida yao binafsi huku wakiwaacha wananchi wakiwa maskini wa kutupwa

No comments:

Post a Comment