About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, October 2, 2011

UCHAGUZI WA UDIWANI KATA YA MATIMIRA CCM WAIBUKA KIDEDEA

                Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Peramiho Anna Mbogo

Na Mwandishi Wetu,Songea
Mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com umefanikiwa kupata matokeo ya uchaguzi wa Udiwani Kata ya Matimila Wilaya ya Songea Vijijini ambapo Chama cha Mapinduzi(CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)walisimamisha wagombea
Matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika Octoba 2 mwaka huu 2011 ambayo yamethibitishwa na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Peramiho ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Songea Vijijini Anna Mbogo ni kuwa mgombea wa nafasi hiyo kutoka CHADEMA ,Eleuterius Kasmir Pili amepata kura 923 na mgombea wa CCM ,Menas Cosmas Komba amepata kura 1386
Kwa matokeo hayo,mtandao huu unaungana na wananchi wote wapenda maendeleo kumpongeza mshindi aliyeibuka kidedea katika uchaguzi huo,pia unatoa pole kwa wale wote waliojeruhiwa kwa namna moja au nyingine katika harakati za uchaguzi huo
Mungu awabariki na kuwapa nguvu wale walioumia kutokana na vurugu zilizojitokeza wakati wa kampeni na wakati wa kusubiri majibu
Mtandao huu una laani vikali nguvu za ziada zilizokuwa zinatumika na vyama vyote viwili ambavyo vilisimamisha wagombea katika uchaguzi huo ulioacha majeruhi zaidi ya 12na kusababisha haki za binadamu kuvurugika na kuchafua demokrasia stahiki
Tunaendelea kuwasiliana na Waandishi wengine waliopo kwenye uchaguzi wa udiwani na ubunge huko Igunga ili tuweze kuwajuza habari za matokeo ya uchaguzi katika maeneo hayo
MWISHO

No comments:

Post a Comment