About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, October 28, 2011

AUAWA BAADA YA KUVAMIWA NA WATU WANAOHISIWA KUWA NI MAJAMBAZI LUPAPILA

Na Gideon Mwakanosya, Songea
NESTORY  Ndomba (20) Mkazi wa Mtaa wa Lupapila katika Manispaa ya Halmashauri ya Songea Mkoa wa Ruvuma amevamiwa na kundi la watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi na kumsababishia kifo papo hapo baada ya kumpiga na kitu kizito kichwani wakati akiwa anaendesha pikipiki akitokea Lizaboni kwenda Lupapila.
Akizungumza na mtandao wa www.stephanomango.blogspot.com jana ofisini kwake Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Naftari Mantamba amesema kuwa tukio hilo limetokea octoba 27 mwa huu majira ya saa 2.30 usiku huko katika eneo la Mtaa wa Londoni uliopo jirani na Lizaboni.
Mantamba amebainisha zaidi kuwa Ndomba anadaiwa kuwa aliuwawa na kundi la watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi ambao wote walijifunga vitambaa vyeusi usoni huku wakiwa wameshika nondo mikononi.
Amesema kuwa majambazi hao baada ya kumkamata walianza kumpiga na kitu kizito kichwani huku wengine wakiendelea kumpekua mifukoni na baadaye walimfunga mikono yote miwili kwa nyuma kiunoni kwa kutumia kamba ya katani ndipo walipomlaza chini na kumnyang’anya pikipiki aina ya sunlug ambayo alikuwa akiiendesha akitokea Lizaboni kwenda Lupapila.
Ameeleza zaidi kuwa Ndomba baada ya kufungwa kamba hiyo majambazi hao walitokomea kusikojulikana na pikipiki hiyo yenye namba za usajili T 846 AYS ambayo thamani yake ni shilingi milioni 1.8 .
Hata hivyo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Mantamba amesema kuwa mpaka sasa majambazi hayo hayajakamatwa na jeshi la Polisi Mkoani humo linaendelea kuyasaka ili yafikishwe mikononi mwa vyombo vya dola.
Wakati huo huo mtu mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Thadei Luambano (45) Mkazi wa Mtaa wa Madizini Kata ya Lizaboni katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea amefariki dunia baada ya kukosa hewa wakati akichimba kisima cha maji huko katika eneo la Jeshi Kambi ya Chabruma mjini Songea.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Naftari Mantamba amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo amedai kuwa lilitokea octoba 27 mwaka huu majira ya saa 10 jioni huko katika kambi ya JWTZ Chabruma ambako Afisa mteule namba 1 wa jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ) Augustino Rashid ndiye aliyetoa taarifa ya tukio hilo katika kituo kikuu cha Polisi cha Songea na Polisi bado inaendelea na uchunguzi juu ya  tukio hilo

No comments:

Post a Comment