About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, November 12, 2011

ASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUMUUA BABA YAKE WILAYANI TUNDURU

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda

Na Augustino Chindiye ,Tunduru

KIJANA wa miaka 21 aliyetambulika kwa jina la Hasan Adam Chimsala anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kumuua Baba yake mzazi Mwalimu mstaafu Mwl. Adamu Isaa Chimsala (60).

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya familia hiyo pamoja na kijana huyo kudaiwa kushindikana kutokana na tabia yake ya unywaji wa pombe na uvutaji bangi wa kupindukiwa  inadaiwa kijana huyo alichukua uamuzi huo kwa kumtuhumu baba yake huyo kuwa amekuwa hampatii matunzo kwa muda mrefu.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael kamuhanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea katika kijiji cha Chemchem Wilayani Tunduru.

Kamanda Kamuhanda aliendelea kufafanua kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Novemba 11 mwaka huu wakati mzee huyo akiwa amejipumzisha kwa ajili ya kusubiri chakula cha jioni.

Alisema wakati marehemu akiwa katika maandalizi hayo ghafla kijana kuyo alimvamia na kuanza kumshambulia kwa kumtoboa na kitu chenye ncha kali kichwani na sehemu mbali mbali za mwili wake.

Taarifa zilizotolewa na Mganga aliyeufanyia mwili wa marehemu Chimsala uchunguzi Dkt.Jeshi Daraja zinasema kuwa kifo hicho kilisababishwa na kutokwa na damu nyingi zilizosababishwa na majeraha hayo.

Alisema marehemu Chimsala alijeruhiwa vibaya kichwani ambako alipasuka fuvu la kichwa chake na kusababisha damu kutoka kwa wingi kupitia masikioni,puani na mdomoni.

Mwisho

No comments:

Post a Comment