About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, November 12, 2011

WANANCHI WATWANGANA KUGOMBEA ARDHI WILAYANI TUNDURU

                             Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Madaha

Na Augustino Chindiye,Tunduru    

MAPIGANO makali ya kugombea Ardhi ya kulima  yamezuka kati ya wakazi wa vijiji vya  Semeni Chikomo Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma na kumjeruhi kwa kukata kata kwa Mapanga mtu mmoja aliyefahamika kwa jina  la Mohamed Abdalah.

Kufuatia tukio hilo majeruhi huyo amelazwa katika Hospitali ya Missioni ya Mbesa baaya ya kujeruhi vibaya sehemu mbali mbali za mwili wake hali iliyo pelekea zaidi ya watu 50 wakazi wa kijiji cha Chikomo Wilayani humo wanatafutwa na Polisi ili waweze kujibu tuhuma hizo zilizotokaka na wananchi wa vijiji hivyo kuanzisha mapigano hayo.

Wakizungumzia tukio hilo kwa nyakati tofauti mbali na kukiri kutokea kwa ugomvi huo madiwani wa Kata za Mtina Mahamudu Katomondo na Kata ya Mbesa , Mohamedi Mtiko kila mmoja wao alitoa lawama kuwa wananchi wa kijiji jirani ndio chanzo cha mgogoro huo.

Upande wa Diwani wa kata ya mtina Katomondo yeye alidai kuwa wananchi wa kijiji cha Chikomo ndio waliofanya makosa ya kuvamia mipaka ya kijiji chake akidai kuwa mpaka unaotenganisha kijiji cha Semeni na Chikomo iliwekwa eneo la ng’ambo ya Mto Lukumbule.

Wakati diwani huyo akitoa madai hayo Diwani wa Kata ya Mbesa Mtiko yeye alidai kuwa na watu watatu waliohusika wakati wa upimaji wa mipaka hiyo mwaka 1978 na wanayo ramani hiyo inayo onesha mipaka ya vijiji hivyo  na kwamba ugomvi uliopo kati ya vijiji hivyo umetokana na wananchi wa kijiji cha Semeni kukaidi kulipa ushuru unaotakiwa kutozwa pindi wakulima wanapovuka mipaka na kwenda kulima kijiji jirani.

Akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo,Katibu tawala wa Wilaya ya Tunduru  Martini Mulwafu mbali na kukiri kuwepo kwa mgogoro huo alisema kuwa ofisi yake imepanga kufanya mazungumzo kati ya viongozi kutoka katika Tarafa, kata na vijiji vinavyohusika na mgogoro huo ili kutafuta ufumbuzi wa kudumu.

No comments:

Post a Comment