About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, November 27, 2011

MAWAKALA WA KUSAMBAZA PEMBEJEO ZA KILIMO TUNDURU WAPATIKANA

                 Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Madaha
Na,Augustino Chindiye TunduruKAMATI inayosimamia ugawaji wa pembejeo za Ruzuku Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma imeteua Mawakala Sita watakao husika katika zoezi la usambazaji wa Mbolea na Mbegu za Mfumo wa Vocha zitakazo tumika katika msimu huu.

Sambamba na kamati hiyo kuwateua mawakala hao baada ya Kampuni zao kufikia viwango vilivyo ainishwa na Wizara husika Mawakala hao wametakiwa kuhakikisha kuwa wanatimiza maelekezo waliyopewa yakiwemo ya kuhakikisha kuwa wameleta Pembejeo hizo kabula ya Desemba 10 mwaka huu na kuanza kuzisambaza katika vijiji vyote vya Wilaya hiyo kabla mvua hazija aanza kunyesha vinginevyo nao watafutwa

Katika zoezi hilo pia kamati hiyo inayo ongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Juma Madaha pia imewafuta uwakala Mawakala 11 bada ya kampuni zao kushindwa kufikia viwango vilivyo bainishwa na Wizara ya Chakula,viwanda na biashara.

Akizungumzia taarifa hiyo Mwenyekiti wa kamti hiyo aliwataja Mawakala walioteuliwa kutoa huduma hiyo kuwa ni Zuberi Namahala, Crispin Mumba, Halima Luambano,Joseph Kalaliche,Augustino Lukosi na Alli Chimwala ambao pamoja na mambo mengine kamati hyo ilijiridhisha kuwa kampuni za wafanyabiashara hao zimekuwa zikifanya kazi hiyo muda wote ikiwa ni tofauti na Mawakala waliofutwa

Dc Madaha aliendelea kueleza kuwa wengi wa mawakala waliofutwa kwa sababu ya kukosa sifa baada ya kamati hiyo kubainika kuwa kampuni zao kutokuwa na ofisi wala maduka ya kutolea huduma hali iliyosababisha wafanyabiahsara hao kujitokeza wakati wa kutafuta Vocha tuna si kutoa huduma kwa wakaulima.

Katika taafa hiyo Dc Madaha aliwataja mawakala hao kuwa ni
Michael Mdete ambaye pamoja na kukosa Duka la kuuzia Pembejeo hizo lakini alikosa sifa kutokana na kuwa na kesi mahakamani baada ya kubainika kuchakachua kwa kugushi na kujipatia Vocha wakati akiwa hajatoa huduma husika kwa waklima.

Wengine ni Bernadetha Methodi Pili aliyekosa sifa za uwakala
kutokana na kuwa ni mke wa Afisa kilimo msaidizi wa Wilaya hiyo ambaye pia ndiyo mratibu mkuu wa huduma hiyo kwa Wakuliwa wa Wilaya hiyo, Craudio Kiwone anaye kabiliwa na tuhuma za kusambaza Mbengu za kienyeji kwa wakulima badala ya mbegu Bora katika msimu uliopita.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo Mawakala wengine walifutwa ni Hadini
Ngunguni,Haridi Kalisinje,Yusuph Kapindo, Mjesye Mjesye,Mohamed
Limbe,Kiyonjo Hasan, Reheme Kalengo na Mchekenae ambao walikosa nafasi hiyo kutokana na kutokuwa na maduka ya kuuzia pembejeo hizo

Akizungumzia mahitaji ya Pembejeo kwa Wakulima wa Wilaya hiyo Afisa Kilimo na Mifugo wa Wilaya ya Tunduru Chiza Marando alisema kuwa jumla ya tani 12 elfu za Mbolea za kupandia na kukuzia pamoja na Tani 400  za Mbegu Bora za mpunga na mahindi ili kukidhi mahitajika kwa Wakulima wa Wilaya hiyo na kuzisambaza  kabla ya kipindi cha mvua

Mwisho

No comments:

Post a Comment