About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, November 27, 2011

PIKIPIKI ZA MCHINA ZAENDELEA KUWAMALIZA WATANZANIA NA WENGINE KUACHWA WAKIWA WALEMAVU

Kamanda wa Polisi Mkoani Ruvuma Michael Kamuhanda Na,Augustino Chindiye Tunduru

MKAZI wa Mjini Tunduru Ramadhani Namadogo (31 ) amefariki dunia baadaya kupata ajali mbaya ya pikipiki aina ya SANLG  yenye namba za usajiri T310 BVM ambayo ilidaiwa kuwa ikiiendesha mwenyewe.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa katika tukio hilo pia ajali hiyo ilimjeruhi rafiki wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Mussa Saanane(27) ambaye hivi sasa amelazwa katika Hospitali ya serikali ya Wilaya ya Tunduru kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Mashuhuda hao waliendelea kueleza kuwa ajali hiyo ilitokea katika mta wa Lambayi Mjini hapa wakati marehemu huyo akirejea nyumbani kwake akiwa anatokea katika maeneo ya Kadewelere ambako ilidaiwa kuwa yeye na majeruhi walienda kupata kinywaji ili kujiliwaza kutokana na ugumu wa maisha.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda
amedhibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kueleza kuwa chanzo cha tukio hilo ni ulevi na kwamba uchunguzi wa Polisi umebaini kuwa Pikipiki hiyo aambayo ilikuwa ni mali ya Marehemu ilikuwa ikiendeshwa na Majeruhi ambaye kwa sasa yupo chini ya ulinzi wa Jeshi hilo.

Akiongea kwa shida majeruhi huyo ambaye amelezwa kitanda namba 12 katika Wodi ya Wanaume katika hospitali hiyo mbali nakukiri kuwa wakati ajali hiyo ikitokea walikuwa wamelewa alikanusha kuwa wakati ajali hiyo inatokea Pikipiki hiyo ilikuwa ikiendeshwa na marehemu pia alikiri kuwa yeye aliendesha pikipiki hiyo wakati yeye na marehemu
wakielekea Kadewele.

Akizungumzia tukio hilo Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Tunduru Dkt. George Chiwangu alisema kuwa kifo hicho kilisababiswa na kutokwa na damu nyingi zilizotokana na kitendo cha kupasuka kwa fuvu la kichwa.

Kuhusu hali ya majeruhi Saanane alisema kuwa hali yake inaendelea vizuri ingawa taarifa zinaonesha kuwa anahitaji kukaa chini ya uangalizi wa maafisa tabibu kwa muda mrefu ili kunusuru maisha yake kufutia majeraha mabaya aliyoyapata kichwani.

Msemaji wa familia hiyo Kaka wa Marehemu Seiph Namadogo alisema
kuwa kifo cha ndugu yake huyo ni cha kawaida na kwamba kinacho
wasikitisha wanafamilia wote ni kitendo cha marehemu kuuza nyumba na kununua piki piki hiyo ili aitumie kwa ajili ya kusanyia abiria akidai kuwa ingeweza kumsaidia kujikwamua kiuchumi kumbe alikuwa anakaribisha umauti wake.

Mwisho

No comments:

Post a Comment