About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, November 17, 2011

TGNP NA DHANA YA UMUHIMU WA KUANZISHA VITUO VYA TAARIFA KWENYE VIKUNDI NA MITANDAO YA KIJAMII

VITUO VYA TAARIFA NA MAALIFA KATIKA JAMII
Na Stephano Mango,Songea
Ni sehemu maalumu ya kukutana kwa lengo la kujifunza na kuhabarishana masuala mbalimbali yanayohusu jamii zetu kwa faida ya vizazi vilivyopo na vijavyo
KWANINI VITUO HIVYO
-Kuleta chachu ya harakati za ukombozi wa mwanamke wa kimapinduzi katika jamii
-Kusaidia ujenzi wa nguvu za pamoja kwa kutumia kukusanya na kusambaza taarifa
-Kuendesha mijadala ya wazi na kuweka kumbukumbu kuhusu mijadala hiyo
-Kufanya uchambuzi na ufuatiliaji wa masuala au kero zinazoikabili jamii husika na kuchukua hatua za pamoja
LENGO KUU
-Kuwawezesha wanaharakati wa ukombozi wa mwanamke wa kimapinduzi,vikundi,mitandao ya jamii kufikia fursa za kupashana,kubadilishana maarifa na taarifa
-Kuongeza hamasa katika masuala yanayohusu haki za binadamu kwa mlengo wa ukombozi wa mwanamke wa kimapinduzi
MALENGO MAHSUSI YA VITUO
-Kuwa na eneo la vituo vya wanawake,vikundi na kuhamasishana ili kuchukua hatua za pamoja kuleta mabadiliko
-Kukita vuguvugu la ukombozi wa mwanamke wa kimapinduzi katika ngazi ya jamii kwa kuwawezesha wanawake na vikundi vya wanaharakati na mitandao kuweka kumbukumbu na kupashana habari
-Kuboresha na kuimarisha mahusiano na kupashana habari kati ya wanaharakati na vikundi ili kupunguza pengo kati ya wanaofaidi taarifa muhimu na wale ambao hawapati taarifa hizo kwa wakati muafaka

No comments:

Post a Comment