About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, November 17, 2011

WANANCHI WATAADHARISHWA UZAGAAJI WA NOTI BANDIA MKOANI RUVUMA

Na Gideon Mwakanosya, Songea

JESHI la polisi Mkoani Ruvuma limewataadharisha wananchi wakiwemo wakulima na wafanyabiashara kuwa makini wanapofanya shughuli zao za kila siku hasa wanapouza mazao au wanaponunua bidhaa za biashara zao kwani katika Mkoa huo noti bandia za shilingi Elfu 5000 na shilingi Elfu 10,000 zimezagaa ambapo kufuatia hali hiyo Polisi imefanikiwa kuwanasa watu wawili wakiwa na noti bandia za shilingi alfu 10 kila mmoja zenye thamani ya shilingi laki 5.

Tahadhali hiyo imetolewa jana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda wakati alipokuwa akiongea na Waandishi wa habari ofisini kwake.

Kamuhanda amewataja wanoshikiliwa na polisi kuwa ni Joseph Kilagi ( 25) na Francis Nkunji (19) wote wakazi wa jijini Dar es salaam ambao walitiwa mbaroni tangu Novemba 13 mwaka huu majira ya saa mbili usiku kwenye kituo kikuu cha mabasi cha Mjini Songea wakiwa wanateremka kwenye basi wakitokea Dar es salaam.

Amesema kuwa askari ambao walikuwa doria kwenye eneo la Kituo cha mabasi waliwakamata watuhumiwa hao wakiwa na noti bandia 50 ambazo kila noti  moja ni shilingi elfu 10 zote zikiwa na thamani ya shilingi laki 5.

Amefafanua zaidi kuwa noti hizo bandia zilizokamatwa zina namba AC.0011601 kila moja na kwamba watuhumiwa walipohojiwa na askari hao waliokuwa doria walidai kuwa wametokea Dar es salaam na wamekuja Songea kufanya biashara ya kununua mahindi.

Kamanda Kamuhanda ameeleza kuwa kwasasa hivi polisi inaendelea kufanya upelelezi kuhusiana na tukio hilo na kwamba watuhumiwa hao watafikishwa Mahakami kujibu shtaka linalowakabili mara tu upelelezi utakapokamilika.

Amewataadhalisha wafanyabiashara wa Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma kuwa wanapofanyabiashara zao kuwa waangalifu pale wanapokutana na noti za shilingi Elfu 5000 na Elfu 10,000ambazo zinadaiwa ndiyo noti bandia zimezagaa kwenye magulio,minada na maeneo mengine ya biashara za jumla na rejareja na kwamba wananchi watakaowagundua watu wenye tabia mbaya ya kusambaza noti bandia watoe taarifa katika kituo chochote cha polisi kilicho karibu.

No comments:

Post a Comment