About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, November 22, 2011

USHIRIKI WAKO KATIKA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA KANDA YA KUSINI NI NGUZO MUHIMU KUIMARISHA TANZANIA HURU

 Mmiliki wa mtandao wa www.stephanomango.blogspot.com, Ndugu Stephano T.Mango anaungana na wanaharakati wengine nchini na nje ya nchi akiwemo Dada yangu Yasinta Ngonyani na Mzee Mbelle kwenye maandalizi ya kuadhimisha siku hizo 16 na kwa wale wote ambao kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao wameshindwa kushiriki siku hizo,Nawapa Pole na tuzidi kuombeana kwani naamini walipenda kushiriki lakini wasihofu naomba waniruhusu niwawakilishe

Mwanabloga Mwenzangu,Mwandishi Mwenzangu wa Habari,Mwalimu Mwenzangu,Mwaharakati Mwenzangu bila kusahau Baba yangu Juma Nyumayo akionyesha bango linaloonyesha ukatili wa kijinsia kwa waandishi wa habari
Na Stephano Mango,Songea
MKOA wa Ruvuma umepewa heshima ya kuadhimisha siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia Kanda ya Kusini inayojumuisha Mikoa ya Iringa,Mbeya,Ruvuma,Lindi na Mtwara kuanzia Tarehe 25/11/2011 hadi 10/12/2011
Katika siku hizo 16 za maadhimisho wadau wanategemea kufanya maandamano,kutoa elimu ya jinsia kwa makundi mbalimbali na kutoa msaada wa sheria katika kata nne zilizopo Halmashauri ya Manispaa ya Songea chni ya kauli mbiu” Miaka 50 ya Uhuru pinga ukatili wa kijinsia kuimarisha Tanzania huru”
Vikundi mbalimbali vya sanaa vitatumbuiza vikiwa na ujumbe lengwa hivyo wadau wote wanatakiwa kuhudhuria kwani ushuhuda mbalimbali wa ukatili wa kijinsia utatolewa na wahusika waliofanyiwa vitendo hivyo

No comments:

Post a Comment