About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, August 31, 2011

MWANAFUNZI ASAKWA KWA KUMUUA MJOMBA WAKE TUNDURU

Na Gideon Mwakanosya,Songea.

JESHI la polisi mkoani Ruvuma linamsaka mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Mtonya iliyopo katika Tarafa ya Nakapanya wilayani ya Tunduru mkoani humo kwa tuhuma za kumuua mjomba wake ambaye alikuwa anaenda kumsaidia mama yake ambaye alikuwa anapigwa na kaka yake.
 
Akizungumza mwandishi wa mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ ofisini kwake kamanda wa polisi wa Mkoa wa Ruvuma Bw.Michael Kamuhanda alisema kuwa tukio hilo la mauaji limetokea jana majira ya saa 8 usiku wakati wa ugomvi baina ya marehemu ambaye jina lake ni Michael Gabriel(23) mkazi wa kijiji hicho na dada yake Marisela Jamadin(27).


Kamanda Kamuhanda alisema kuwa inadaiwa siku ya tukio hilo katika kijiji hicho cha Mtonya Gabriel aliuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na mtoto wa dada yake huyo Agrey Emmanuel(14) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Mtonya wilayani humo na baada ya kugundua kuwa ameua alikimbia na kutokomea kusikojulikana.
Kamanda Kamuhanda alisema kuwa mwanafunzi huyo Agrey anatarajia kufanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi  utakaofanyika nchini kote mwezi ujao na hivyo jeshi la polisi mkoani humu linaendelea kumsaka kuhusiana na tuhuma hizo na uchunguzi unaendelea kuhusiana na tukio hilo na hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa.
Hata hivyo kamada Kamuhanda alisema kuwa chanzo cha ugomvi huo ambao umepelekea  Gabriel kuhuwawa na mpwa wake bado hakijajulikana licha ya kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment