About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, January 24, 2012

WASAFIRISHAJI WA MIZIGO WAULALAMIKIA UONGOZI WA MANISPAA SONGEA

Na Stephano Mango,Songea
WASAFIRISHAJI wa mizigo wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wameulalamikia uongozi wa Manispaa hiyo kwa kitendo cha kuwazuia  kuingia na magari ya mizigo katikati ya mji wafanyabiashara wachache huku wengine wakiingia na magari ya mizigo bila kuchukuliwa hatua yoyote
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na waandishi wa habari jana mjini hapa,wasafirishaji hao ambao waliomba majina yao yahifadhiwe,walisema kuwa kitendo kinachofanywa na Uongozi wa Manispaa  ni cha uonevu kwa sababu wamewazuia kuingia na magari katikati ya mji bila kuwatengea maeneo mengine yenye miundombinu mizuri ya maji,choo,ofisi na umeme
Walisema kuwa wasafirishaji wengi wana ofisi zao katikati ya mji ambazo zinahuduma zote muhimu ambapo uwepo wake unawasaidia wateja wao kuweza kuchukua mizigo yao kwa urahisi na kwa bei ndogo hivyo uwepo wa ofisi mbali kinawaletea usumbufu wananchi ambao ni wateja muhimu kwao
Walieleza kuwa pamoja na kupokea maelekezo ya Viongozi wa Manispaa kuwa magari yanayotakiwa kuingia mjini yasizidi tani 10 lakini kuna baadhi ya magari yanaingia na hayachukuliwi hatua yoyote na maagizo ya Viongozi hao yanabadilika kila wanavyoamua bila kujali usumbufu unaojitokeza kwani awali walituambia gari za tani 10 ndizo zinazopaswa kuingia mjini lakini baada ya wiki moja kwisha wanatuambia gari za 9 ndizo zinapaswa kuingia mjini
Walisema kuwa kutokana na usumbufu huo Wasafirishaji wanalazimika kupandisha bei ya kusafirisha mizigo na kusababisha wananchi kupandishiwa bei ya bidhaa kwani kila inachokifanya Serikali dhidi ya wafanyabiasha mwisho wa siku gharama hizo zote zinapaswa kulipwa na mwananchi mnyonge na kusababisha gharama za maisha kupanda sana
Walieleza zaidi kuwa miji mingine yote  nchini gari zinaingia mwisho gari za tani 10 ili kuweza kulinda barabara za ndani ya mji na kupunguza msongamano katikati ya mji lakini hapa tunashangaa kuambiwa kuwa gari zinazotakiwa kuingia mjini mwisho za tani 9 tena ziingie usiku wakati gari hizo hazipo
Walifafanua kuwa wameelekezwa kuanzia disemba 31 mwaka 2011 walitakiwa kutoingia kwenye barabara za mjini badala yake waishie na kushusha mizigo kwenye uwanja wa nanenane na sio vinginevyo wakati eneo hilo ni uwanja uwezi kujenga choo,hakuna huduma ya umeme,ofisi za wasafirishaji ,maji,chakula hivyo wametupatia wakati mgumu sana wa kuitunza mizigo ya watu na utunzaji wa mazingira
Walisema kuwa maagizo ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea yamejaa utata hata wanaopaswa kusimamia maagizo yake wamekuwa wakishindwa kuyazuia magari yote kuingia katikati ya mji na ndio maana magari mengine yamekuwa yakipita bila maelezo yoyote kutokana na udhaifu wa viongozi hao
Awali kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa Nachoa Zakaria,Afisa Biashara wa Manispaa hiyo  Kelvin Challe aliwaandikia barua tarehe 12 Disemba,2011 wasafirishaji yenye kumb,na,SO/MC/T.10/14/11 kuhusu kusitisha kuingia magari ya mizigo yanayozidi tani 10 ndani ya barabara za Manispaa kuanzia Disemba 31,2011
Baada ya agizo hilo kuhojiwa na Wasafirishaji kutokana na kugubikwa na utata Uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea   tarehe 9 Januari 2011, iliwaandikia tena wasafirishaji barua na kusaini na Kelvin Challe yenye Kumb.Na.SO/MC/T.10/14/11/17 yenye kichwa cha habari Ufafanuzi wa kina juu ya zoezi la kusitisha kuingiza magari ya mizigo kuanzia tani 10 ndani ya barabara za Manispaa Songea Kuanzia tarehe 31/12/2011
Sehemu ya barua hiyo inasema…..magari  yanayoruhusiwa  ni magari yenye uzito wa kuanzia tani 9 tu.Magari yenye  uzito zaidi ya tani 9 yanatakiwa kushusha mizigo katika uwanja wa nanenane,hivyo unatakiwa kuzingatia na kutekeleza maamuzi hayo
Jitihada za kumpata Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea aweze kujibu malalamiko ya wasafirishaji  Nachoa Zakaria ziligonga mwamba baada ya kuambiwa na mhudumu wa Ofisi yake kuwa yupo kwenye vikao ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na alipotafutwa kwenye simu yake ya kiganjani,simu iliita bila kupokelewa
MWISHO

No comments:

Post a Comment