About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, February 19, 2012

MKUU WA MASOKO MANISPAA YA SONGEA SALUM HOMERA AONYA MWENENDO WA NCHI

MKUU WA MASOKO HALMASHAURI YA MANISPAA YA SONGEA SALUM HOMERA
Na Stephano Mango,Songea
SERIKALI imetakiwa kuona umuhimu wa kurudisha Azimio la Arusha ili kuweza kuwajengea watanzania pamoja na viongozi maadili ya uzalendo katika kuijenga Tanzania miaka 50 ya uhuru ijayo
Wito huo umetolewa jana na Mkuu wa Masoko wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Salum Homera ofisini kwake alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa
Homera alisema kuwa viongozi wengi wa sasa hawana maadili ya uongozi na wamekosa uzalendo wa kulitumikia taifa kwa moyo wote jambo ambalo linasababisha viongozi hao kushindwa kuwajibika ipasavyo katika ofisi za umma na mara nyingine kukumbwa na kashfa ya rushwa na ufisadi
Alisema kuwa kurudishwa kwa azimio la Arusha kutawafanya viongozi kufanya kazi kwa kufuata maadili na uzalendo wan chi kwa kuzitunza na kuzitumia rasilimali za nchi vizuri kwa faida ya watanzania wote na kuwasaidia watanzania kuwa na maendeleo mazuri
Alisema watanzania watakapo kuwa na maendeleo mazuri wataipenda nchi yao na viongozi wao kwani kwa pamoja watasaidiana kuijenga Tanzania yenye afya kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo
Alifafanua kuwa kila siku Serikali imekuwa ikishuka heshima yake kama mhimili muhimu wa uongozi kwa ujenzi wan chi makini kutokana na kukiukwa kwa misingi imara ya Azimio la Arusha na kwamba kutokurirudisha kutaendelea kushusha heshima ya Serikali na viongozi wake
Alisema kuwa kwa hali ya nchi ya sasa, ni muhimu vijana wanaomaliza kidato cha nne wakaenda kupata mafunzo mbalimbali ya ukakamavu na ya uzalendo kwa nchi yao katika Jeshi la Kujenga Taifa JKT, jambo ambalo litapunguza migomo katika vyuo vikuu kwa sababu watakuwa wamepata mafunzo ya uzalendo na hivyo kuwafanya kuwa na utaifa mbele badala ya kuwa na maslahi binafsi
Alisema kuwa kwa kufanya hivyo watanzania watakapo kuwa kwenye maeneo yao ya kazi watazingatia utaifa kwani hata wafanyabiashara watashindwa kujipangia wao bei za bidhaa kiholela na kuwafanya watanzania wanyonge wapate tabu katika maisha au kuiraumu Serikali kuwa imeshindwa kuzuia mfumuko wa bei holela
Alieleza zaidi kuwa uchakachuaji wa fedha nyingi za umma katika miradi ya wananchi kunatokana na wasimamizi wa fedha hizo kutokuwa na uzalendo stahiki wa kuijenga nchi yao hivyo kwa kupitia JKT hali hiyo inaweza ikapungua na hatimaye kwisha kabisa ustawi wa nchi yetu
MWISHO
 

No comments:

Post a Comment