About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, July 3, 2012

CHADEMA RUVUMA KUFANYA MKUTANO MKUBWA WA HADHARA LEO MCHANA

Na Mwandishi Wetu, Songea

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Ruvuma leo tarehe 4/7/2012 majira ya saa nane kinatarajia kufanya mkutano mkubwa wa hadhara katika Viwanja vya Soko la Samaki la zamani (Shule ya Msingi Mfaranyaki)

Taarifa zilizopatikana mjini hapa jana na kuthibitishwa na Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mjini Joseph Fuime zimeeleza kuwa mkutano huo utahutubiwa na viongozi wa ngazi mbalimbali wa Chadema kutoka ndani ya mkoa wa Ruvuma

Fuime alisema lengo kuu ni kuimarisha chama na kukemea mambo ambayo yanaashiria ukandamizaji wa haki za wanyonge kunakofanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi

Hata hivyo, alitoa wito kwa wanachama na wananchi wote kujitokeza kwa wingi katika mkutano huo ili kuweza kusikia sera za Chadema na maovu yanayofanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi
MWISHO

No comments:

Post a Comment