About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, September 8, 2012

WAZIRI LWENGE AICHARUKIA KAMPUNI YA PROGRESSIVE


Na, Steven Augustino, Tunduru

SERIKALI imetoa nafasi ya mwisho ya matazamio kwa Mkandarasi anayejenga kwa kiwango cha Lami Barabara ya kutoka Namtumbo kwenda Tunduru yenye urefu wa zaidi ya Kilometa 188 zitakazo ghalimu zaidi ya shilingi Bilioni. 180.66 huku ikiahidi kuchukua hatua kali kwa mkandarasi huyo kampuni ya progressive Constraction

Kauli hiyo iliyo onesha kuwa mkuki mkali kwa viongozi wa kampuni hiyo ilitolewa na Naibu waziri wa Ujenzi Eng. Gerson Lwenge wakati akiongea katika majumuisho katika Ukumbi wa halmashauri ya Wilaya ya Tunduru baada ya kukamilisha ziara yake ya kikazi Mkoani Ruvuma na kuongea na wakandarasi wa kamuni hiyo ambapo pamoja na mambo mengine alionesha kushangazwa na kusuasua kwa mradi hio.

,,Uvumilivu wa Serikali kwa kampuni yenu umefikia kikomo na hatuendelea kuwa wazembe wa kuzibeba kampuni za aina hiyo ambayo hadi sasa imetimiza miezi 18 kazini bila kuonesha uhai wowote,, alisema kwa ukali Eng. Lwenge na kuongeza kuwa hali hiyo imetokana na kujionea ubabaishaji huo na ajaridhika na kasi ya ujenzi wa barabara hiyo na kwamba Serikali itachukua hatua dhidi ya Mkandarasi na Msimamizi wa Kampuni hiyo.

Aidha Eng. Lwenge baada ya kukerwa na hali hiyo aliwaahidi wanachi wa Wilaya ya Tunduru kuwa atapeleka kero iliyosababishwa na kampuni hiyo katika vikao vyenye maamuzi ili kuangalia utaratibu wa kukatisha mkataba wao.

Alisema kuwa kampuni ya Progressive Constraction ilisaini mkataba wa kukamirisha mradi huo katika kipindi cha miezi 27 iwe imekamilisha ujenzi wake lakini hadi sasa takwimu zinaonyesha kuwa katika kipindi chote hicho kazi zilizofanyika ni uwiano wa asilimia 4% tu za ujenzi wa Mradi huo hali inayo onesha kuwa ili mradi huo uweze kukamilika kwa wakati wa miezi 9 iliyobakia inahitajika kufanyika miujiza.

Alisema mradi huo uliogawanywa katika vipande vitatu na kuainisha thamani zake ni Tunduru Matemanga Kilometa 58.70 Shilingi Bilioni. 63.41 kilipangwa kukabidhiwa mwezi Julai 2013, Matemanga Kilimasera kilometa 68.20 chenye thamani ya Shilingi Bilioni. 64.02 kilipangwa kukabidhiwa mwezi Mei 2013 na Kilimasera Namtumbo Kilometa 60.70 Chenye thamani ya Shilingi Bilioni.53.23 kilipangwa kukamilika mwezi machi 2013.

Aidha Eng. Lwenge pia alitumia nafasi hiyo kuzipongeza Kampuni za SOGEA SATOM anaejenga Bara bara za Songea - Namtumbo kilometa 67.00 utakao ghalimu Shilingi Bilioni.62.88 na … inayojenga Barabara ya Peramiho - Mbinga kilometa 78.00 wenye thamani ya shilingi Bilioni.79.81 kuwa inaendelea vizuri na akaongeza kwa kuonesha mashaka ya mdororo wa ujenzi wa Barabara ya Tunduru - Namtumbo kuwa huenda mradi huo ukapitwa na miradi mipya ya Barabara za Tunduru Mtambaswala Kilometa 202.5, Shilingi Bilioni.240.858 na Mbinga - Mbambabey kilometa 66.00 utakao ghalimu shilingi Bilioni.2.90.

Awali akisoma taarifa ya maendeleo ya Wilaya ya Tunduru kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo Chande Nalicho, Afisa Tawala wa wilaya hiyo Martin Mulwafu pamoja na kueleza changamoto mbalimbali ambazo zimekuwa zikiikabili Wilaya hiyo wakati wa kutekeleza miradi ya Barabara na Ujenzi alisema kuwa halmashauri hiyo imepanga kutumia jumla ya shilingi 1,097,920,000/.

Alisema fedha hizo zilizopangwa kwa ajili ya kufanya matengenezo ya maeneo korofi katika barabara za Changarawe,vumbi na kilo meta 3 za Lami nyepesi, kujenga madaraja kwa ajili ya kufanya matengenezo ya barabara za Tunduru mjini Tsh.675,780 Milioni zitatolewa na mfuko wa barabara, Tsh.428.000 Milioni zitatolewa na mpango wa kuzipatia ruzuku serikali za mitaa (LGCDG) na (CDG).

Akiongea kwa niaba ya wajumbe walioshirika katika mazungumzo hayo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mustafa Bora aliwataka Mawaziri kumsaidia Rais katika utekelezaji wa majukumu yao ili kukifanya chama chake kutimiza ahadi zilizopangwa kutekelezwa katika ilani yake ya mwaka 2010-2015 huku Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo Ephraem Ole Nguyaine akimaliza kwa kuwa kumbusha na kuwa karibisha Viongozi wa Kitaifa kutembelea Tunduru iliyopo pembezoni ili kutoa msukumo na kuwaondoa wananchi dhana waliyo ijenga kuwa viongozi wao wamekuwa wakifika nyakati za kampeni tu.

Akiongea kwa niaba ya Kampuni hiyo, Meneja mshauri wa kampuni ya Progressive Constraction Marid Poli pamoja na kueleza changamoto lukuki zikiwemo za kampuni kutokuwa na wataalamu na watumishi wakutosha ndio kikwazo kwa kampuni kutekeleza wajibu wake. aliiomba Serikali kutokatisha mkataba huo na kuahidi kuwa kazi hiyo itaisha kwa wakati na kwamba tayali wamekwisha jipanga kuhakikisha kuwa shughuli zote zinakwisha katika kipindi cha miezi 9 iliyobakia.

Akiwa Ruvuma Eng, Lwenge alianza kwa kutembelea kivuko cha Mto Luhuhu mpakani mwa wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma na Ludewa iliyopo mkoa wa Njombe ambako alisema kuwa Serikali ipo kwenye mchakato wa kuhakikisha inajenga Daraja na bwawa litakalosaidia kilimo cha katika mto huo.
Mwisho

No comments:

Post a Comment