About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, March 7, 2013

WANAKONGANO WATAKIWA KUJITUMA KATIKA UZALISHAJI WA UYOGA



Na,Mwandishi Wetu , Songea
WANAKONGANO wa Uyoga Songea wametakiwa kujishughulisha kwa kasi na kujituma katika kilimo cha uyoga ili kuweza kuongeza uzalishaji wa zao hilo ili walaji waupate kwa wingi kwa mahitaji mbalimbali katika Jamii

Wito huo umetolewa jana na  Mkuu wa Wilaya ya Songea Joseph Mkirikiti kwenye ukumbi wa Saccos ya Walimu Songea Mjini wakati akiwahutubia Wanakongano na wageni waalikwa kwenye hafla fupi ya kuikabidhi hundi ya shilingi milioni nane Kongano la Uyoga Songea

Mkirikiti alisema kuwa  Kongano la Uyoga Songea  linapaswa kuwa chachu ya kujiimarisha katika uzalishaji wa zao la Uyoga  kwa lengo la kuongeza lishe na kipato miongoni mwa Jamii kama vile malengo yake ya kuanzishwa yanavyosema

Alisema kuwa hadi sasa Kongano hili limethubutu kufanya jambo  la kimaendeleo ambalo leo limetukutanisha katika ukumbi huu likiwa na malengo ya kuiwezesha jamii kupata lishe bora na kipato miongoni mwao

Awali akizungumza na Wanakongano hao Mratibu wa Kongano Nchini kutoka Tume ya Sayansi na Teknologia Omary Bakari alisema kuwa (Songea Mushroom Cluster ) Kongano la Uyoga Songea limeonyesha mfano wa kuigwa kwani mara baada ya kupata mafunzo ya uwezeshaji waliweka mpango kazi ambao leo umezaa matunda stahiki

Bakari alisema kuwa mpango huo umeletewa fedha ya shilingi milioni nane kutoka Tume ya Sayansi na Tecknologia ili uweze kutekelezwa na kufikia mafanikio yaliyokusudiwa kadri ya shughuli zilizopangwa kwenye mpango kazi

Awali akizungumza kwenye hafla hiyo Katibu Mtendaji wa Kongano la Uyoga Songea Stephano Mango alisema kuwa haikuwa gazi rahisi kutengeneza mpango huo wa kuiwezesha Kongano ili liweze kusonga mbele

Alisema kuwa mpango huo utaiwezesha Kongano kuimarika na kuongeza uzalishaji wa uyoga kwa sababu fedha iliyofika itasaidia kutatua vikwazo ambavyo vinaisumbua Kongano vikiwemo vya uharibifu wa Vimeng’enya, wadudu waharibifu,zana duni za kilimo na kuhifadhia uyoga, elimu duni ya kumbukumbu

Mango alisema kuwa mpango huo ni wa miezi 18 na kwamba umegawanyika katika vipengele vitatu vya  uhamasishaji ,muda mfupi na muda mrefu ili malengo yatimie
MWISHO

No comments:

Post a Comment