About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, May 17, 2013

ALIYEKUWA DEREVA WA HALMASHAURI YA NAMTUMBO AKAMATWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUKUTWA NA MENO YA TEMBO.




Na Gideon Mwakanosya,Songea
JESHI la polisi mkoani Ruvuma kwa kushirikiana na idara ya maliasili mkoani humo wamemtia mbaroni aliyekuwa dereva wa halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Buruhani Mtini [48]mkazi wa Bombambili Manispaa ya Songea kwa tuhuma za kukutwa na vipande nane vya meno ya Tembo yenye uzito wa jumla ya kilo 18 vyenye thamani ya shilingi milioni 48 yakiwa ndani ya sanduku wakati akiyasafirisha kwa kutumia baiskeri.

 Habari zilizopatikana jana mjini Songea ambazo zimethibitishwa na kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki zimesema kuwa tukio hilo limetokea mei 10 mwaka huu majira ya saa 4.45 asubuhi huko katika eneo la Lwinga lililopo Namtumbo mjini karibu na kituo kikuu cha mabasi .

Alisema kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio kwenye eneo la lwinga chini ya kituo kikuu cha mabasi maafisa wa idara ya maliasili kwa kushirikiana na askari polisi wa wilaya ya Namtumbo walifanikiwa kumkamata Mtini akiwa na vipande nane vya meno ya tembo yenye uzito wa kilo 18 ambayo inadaiwa inatokana na kuwawa kwa tembo wawili wenye thamani ya USA Dola 15,000 kwa kila mmoja na kufanya jumla ya tembo wote wawili USA Dola 30,000 sawa na thamani ya Tanzania Tsh 48,000,000.

 Alifafanua zaidi kuwa Mtini alikamatwa akiwa na meno ya tembo ambayo alikuwa ameyafunga ndani ya sanduku akiwa anayasafirisha kwa kutumia baiskeri kwenda kwenye kituo kikuu cha mabasi ya mjini Namtumbo ambako yalikuwa yanatarajiwa kupelekwa Songea mjini ili yaanze tena kupelekwa jijini Dare esalaam.

 Alibainisha zaida kuwa mtuhumiwa Mtini baada ya kukamatwa wakati wa kumpekua alikutwa na msumeno mdogo ambao ulikutwa umehifadhiwa ndani ya sanduku ambao unasadikiwa ndio uliyotumika kukatia meno hayo na mzani mdogo [SPRING BALANCE]ambao unadaiwa ni kwa ajili ya kupimia uzito wa meno hayo.

Kamanda Nsimeki aliongeza kuwa vilevile walipoendelea kumpekua kwenye mifuko ya nguo alizo vaa walimkuta akiwa na kitambulisho cha utumishi kinachoonyesha kuwa ni mfanyakazi wa halmashauri wa wilaya ya Namtumbo aliyeajiriwa kama dereva lakini taarifa zaidi kutoka ndani ya halmashauri ya wilaya hiyo zinadai kuwa alisha achishwa kazi siku nyingi baada ya kupata ajari ambayo ilisababisha kifo akiwa na gari la halmashauri hiyo tangu mwaka 2006.

Hata hivyo kamanda Nsimeki alisema kuwa kufuatia tukio hilo polisi kwa kushirikiana na idara ya maliasili inaendelea kufanya upelelezi wa kina na utakapo kamilika mtuhumiwa Mtini atafikishwa mahakamani kujibu shistaka linalo mkabili.
           MWISHO.
Top of Form
Bottom of Form
Top of Form
Bottom of Form
Top of Form
Bottom of Form
Top of Form
Bottom of Form

No comments:

Post a Comment