About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, May 10, 2013

MFUMO WA KONGANO BUNIFU SULUHISHO LA MAENDELEO

Na, Mwandishi Wetu, Morogoro
MFUMO wa kongano bunifu umetajwa kama mkombozi utakaoleta maendeleo endelevu Tanzania kama utazingatiwa na wadau mbalimbali.
Meneja wa Programu ya Fanikiwa Kibiashara (BDG) ambayo inafanya kazi chini ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Sosthenes Sambua, alitoa kauli hiyo mjini hapa jana wakati wa mafunzo ya kuwezesha kongano mbalimbali nchini kujenga ubunifu na ushindani.

Mafunzo hayo ya siku nne yanayoendelea mjini hapa yanaendeshwa na Scandnavian Institute for Competitiveness and Development (SICD) pamoja na Pan African Competitiveness Forum (PACF) kwa kushirikiana na BDG, Programu inayoendeshwa chini ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Sambua ambaye alikuwa mmoja wa wakufunzi katika mafunzo hayo, amewaambia waandishi wa habari kuwa mfumo wa kongano una nafasi kubwa ya kuleta hali bora ya maisha kwa Watanzania kwa kuwa unashirikisha nguzo tatu muhimu katika uundwaji wake ambazo ni serikali, wanataaluma au watafiti na wazalishaji katika jamii husika.

Alisema katika ushirikiano huo kongano huja na ubunifu na njia mpya za uzalishaji na kujenga ushindani si tu wa ndani bali pia nje ya nchi, hivyo kuleta maendeleo.

Akitoa mfano wa mataifa mengine alisema nchi kama Sweden, Ujerumani, Italia, Hispania, na Uholanzi zimekuwa zikitumia mfumo huu wa kongano kwa zaidi ya miaka 20 na kuwa bado wanaendelea kuwekeza katika mfumo huo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya washiriki katika mafunzo hayo walitoa shukrani kwa waandaaji wa mafunzo hayo na kuahidi kufanyia kazi ujuzi watakaopata kuimarisha kongano zao.

No comments:

Post a Comment