About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, June 11, 2013

CHADEMA YAIFYATUA CCM KWA KUPATA USHINDI WA KISHINDO MKOANI RUVUMA


 Mwenyekiti wa Kanda ya Kusini ya Chadema ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Ruvuma Joseph Fuime akiwahutubia mamia ya wananchi wa Kata ya Mkako kwenye mkutano wa Ufungaji wa kampeni ya Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kitongoji  cha Masangu kijiji cha Amani Makolo, Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma
 Mgombea aliyeshinda Uenyekiti wa Kitongoji cha Masangu kijiji cha Amani Makolo, Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma Nestory Komba wakati akiomba kura
 Kutoka kushoni ni Diwani wa Viti Maalum wilaya ya Mbinga Anastasia Magubike, Diwani wa Vitimaalum Manispaa ya Songea Rhoda Komba, na watatu ni Katibu wa Kanda ya Kusini ya Chadema Edmund Nditi wakifuatilia kwa makini hotuba ya Ufungaji wa Kampeni hizo juzi kutoka kwa Mwenyekiti wa Kanda ya Kusini ya Chadema ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Ruvuma Joseph Fuime
 Katibu wa Kanda ya Kusini ya Chadema Edmund Nditi
akiwahutubia mamia ya wananchi wa Kata ya Mkako kwenye mkutano wa Ufungaji wa kampeni zilizofanyika Kitongoji cha Masangu
 Baadhi ya Viongozi wa Jimbo na Wilaya ya Mbinga wakifuatilia Kampeni hizo juzi
Na  Stephano Mango, Songea
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)  Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma kimepata ushindi mnono kabisa kwa kukibwaga Chama  cha Mapinduzi ( CCM ) kwenye uchaguzi mdogo wa Kitongoji  cha Masangu kijiji cha Amani Makolo,Kata ya Mkako
Akitangaza matokeo hayo jana Msimamizi Msaidizi wa uchaguzi huo Bahati Liholile Haule alisema kuwa wapiga kura waliojiandikisha katika uchaguzi huo walikuwa ni 110, waliojitokeza kupiga kura walikuwa 103 ambapo hakuna kura zilizoharibika
Haule alisema kuwa katika uchaguzi huo Vyama viwili vya Siasa vilisimamisha wagombea ambapo kwa Chama cha Mapinduzi ( Ccm) kilimsimamisha Alto Ngonyani kugombea nafasi hiyo na kwa upande wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( Chadema) kilimsimamisha Nestory Komba kugombea nafasi hiyo ya Kitongoji
Alifafanua kuwa katika uchaguzi huo ambao ulitawaliwa na amani kubwa matokeo  ya mgombea wa Ccm yalikuwa ni kura 45 na mgombea wa Chadema alipata kura 58
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kanda ya Kusini ya Chadema ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( Chadema) Mkoa wa Ruvuma Joseph Fuime alisema kuwa ushindi ulikuwa mgumu , licha ya Serikali ya Ccm kutengeneza mazingira mfu ya kujipatia ushindi lakini walishindwa na nguvu ya umma ambayo ilijikita wazi katika kampeni ya kimkakati makini wa kujipatia ushindi wa kumpata kiongozi bora
Fuime alisema kuwa ushindi huo ni salamu tosha kwa watawala wa Ccm kuwa wananchi hawaitaji maneno yenye kutia matumaini bali wanachoitaji sera stahiki za kuwaondoa katika minyororo ya maumivu ya maisha kutoka na gharama za uendeshaji wa maisha yao kupanda
Alifafanua kuwa Mkoa wa Ruvuma umejaliwa kuwa na Rasilimali nyingi sana ikiwemo Makaa ya Mawe yaliyopo mita chache kutoka ambapo uchaguzi umefanyika lakini Rasilimali hizo zimekuwa hazitumiki kuwanufaisha wananchi wake
Alisema kuwa wanaonufaika na Rasilimali hizo ni Viongozi wa kifisadi wanaotokana na Ccm akiwamo Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mashariki Gaudence Kayombo na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga na ushahidi upo wazi ukifika katika Ofisi ya Mwenyekiti wa Kijiji,Mwenyekiti wa Kitongoji au Kwa Afisa Mtendaji wa Kata ya Mkako
Alifafanua kuwa ukifika kwenye ofisi hizo utakutana na saini zao hapo na ujumbe wao ambao una malengo yenye utata dhiti ya maeneo ambayo yana Rasilimali muhimu ambazo zingetumika vizuri zingeweza kusababisha wananchi waishi maisha ambayo Mungu anayapenda
“Ukifika katika Ofisi hizo utakuta Viongozi hao wametembelea Ofisi hizo mara nyingi kuliko maeneo mengine ambayo yana kabiliwa na changamoto nyingi na wananchi wanawahitaji kwa ajili ya kuwaongoza katika kutatua shida  zao lakini cha ajabu huwa awatembelei maeneo hayo mpaka muda wao wa Uongozi unakwisha
Mwenyekiti huyo alimalizia kwa kusema kwa nafasi hiyo anawashukuru wananchi kwa kutambua sera nzuri ambazo zinapaswa kutekelezwa na Kiongozi mzuri na pia kwa kupuuza ghiriba zilizo zeeka za Ccm na kutoa ujumbe kwa watawala katika chaguzi za kuelekea mwaka 2014 na 2015 ili kuleta matumaini na mustakabari mpya wa Taifa salama
MWISHO
 

Stephano Theofrida Mango 
 P.O.BOX 835, SONGEA, RUVUMA- TANZANIA.
SIMU: 0755-335051, 0715-335051, 0784-335051, 0778-335051,
 E-MAIL;stephano12mango@yahoo.com  www.stephanomango.blogspot.com

No comments:

Post a Comment