About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, June 24, 2013

TGNP WAFUNGA MITAMBO YA KISASA MOROGORO

 Afisa Habari na Mawasiliano wa TGNP Lilian Kittunga akifundisha Program Maalum ya Kutumia mawasiliano miongoni mwa Vikundi vya Sauti ya Jamii Kituo cha Taarifa na Maarifa
Na, Mwandishi Wetu, Morogoro

MTANDAO wa Jinsia nchini (TGNP), umepanua mawasiliano kwa kutoa na kufunga mitambo ya kisasa ya mawasiliano kwenye vituo vya taarifa na maarifa ya jamii chini ya wanaharakati wa maendeleo katika mikoa mitano nchini.

Hayo yamebainishwa mwishoni mwa wiki wilayani Morogoro na Ofisa Programu ya Utetezi na Mawasiliano na Habari TGNP, Deogratius Temba wakati akikabidhi mtambo wa aina hiyo kwenye kituo cha wanaharakati Mkabarani.

Alisema dhamira ya wananchi kuwezeshwa mtambo huo ni kuzinduliwa mradi wa ‘Sauti ya Jamii’ ambapo hapo utaitwa 'Sauti ya Jamii Mkambarani', ili kuongeza nguvu ya pamoja katika mapambano ya mabadiliko chanya ya maendeleo kwa kuhabarishana.

“Kuanzishwa kwa ‘Sauti ya Jamii’ na kutolewa kwa mtambo huu ni matokeo ya changamoto zilizojitokeza kwenye matamasha na mafunzo yaliyotolewa kwa jamii na TGNP hivi karibuni,” alisema Temba.

Alisema malengo ya kituo ni kumwezesha mwanawake na jamii kujikwamua kifikra, kiuchumi, kisiasa na kumharakishia maendeleo kutoka katika mfumo dume unaomzunguka.

Akitoa nasaha juu ya uanaharakati bora, Diwani wa Kata ya Mkambarani, Daniel Shawa, aliwataka wanaharakati kufuata sheria, taratibu na kanuni zilizopo ili waheshimike na kuthaminiwa katika jamii wanayoitetea.

Mtambo huo ulioambatana na vifaa vya teknolojia ya kisasa ikiwemo kompyuta, ‘printer’ na chombo cha kuhifadhia vimetolewa Mkambarani wilayani Morogoro, Kisarawe mkoani Pwani, Kishapu mkoani Shinyanga, Songea na jijini Dar es Salaam.
MWISHO

No comments:

Post a Comment