About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, July 5, 2013

LOWASSA ADAIWA KUCHEZA KALATA VIZURI KASHFA YA RISHMOND


Aliyekuwa kuwa Waziro Mkuu, Edward Lowassa akiteta jambo na aliyekuwa Spika wa Bunge la Tisa Samwel Sitta



WAZIRI Mkuu aliyejihudhuru Edward Lowassa mwaka 2006 kwa tuhuma za ufisadi kupitia kampuni ya kufua umeme Richmoind, sasa imebainika kuwa alitolewa mbuzi wa kafara baada ya mitambo hiyo kuzinduliwa na Rais wa Marekani Barck Obama ikiwa na jina la Symbion.


Kwanza waliosuka mpango wa kumchafua Lowassa walisema Richmond ni Kampuni ya mfukoni, na ni ya Lowassa, haina uwezo wa kuzalisha Umeme wala kufunga balbu.

Wakasema Dowans ni pacha na Richmond, Wapambe wachache wakasema Serikali isinunue Mitambo hiyo maana haifai, sasa ni Simbyon Power.

Mitambo hiyo hiyo ndiyo imezinduliwa juzi na Obama, je?amezindua mitambo mibovu isio na uwezo wa kuzalisha Umeme wala kufunga balbu? je Obama naye ni fisadi? au kwasababu akina fulani wakisema ndimi zao zinaaminika zaidi ya wengine?

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanasema kuwa Lowassa alikuwa anaona mbali sana na alikuwa sahihi, ila alihujumiwa kisiasa tu na wasioitakia Nchi yetu mema bali kwa maslahi yao maana mitambo hiyo wakati inazinduliwa mpaka Rais Jakaya Kikwete na vionmgozi wengine wa nchi walionekana wakipiga makofi!

No comments:

Post a Comment