About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, January 30, 2015

MWANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA SONGEA AJINYONGA




NA STEPHANO MANGO,SONGEA


MWANAFUNZI wa Kidatao cha kwanza katika shule ya Sekondari ya msamala iliyopo manispaa ya Songea mkoani Ruvuma James Mbano (16) amekutwa chumbani kwake alikokuwa analala amejinyonga kwa kutumia kamba aina ya Katani kwa kuifunga kwenye kenchi za paa la nyumba ya Mjomba wake.
 

Habari zilizopatikana jana mjini Songea ambazo zimethibitishwa na kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Yahaya Athumani zimesema kuwa tukio hilo limetokea Janua 29 mwaka majira ya saa 1030 za jioni huko katika eneo la Mkuzo Ruwawasi kata ya Msamala manispaa ya Songea.
 

Alisema kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio James alikutwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya katani ambayo ilifungwa kwenye kenchi la paa katika chumba alichokuwa analala ambapo tukio hilo liligunduliwa na mjomba wake Castory Silvesta (37) ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi mfaranyaki.

Alieleza zaidi kuwa Mwalimu Silvesta baada ya kugundua tukio hilo alitoa taarifa katika kituo kikuu cha Polisi  cha mjini Songea ambapo baadae timu ya askari wa idara ya upelelezi Mkoa wakiongozana na Dkt. Toka hospitali ya Mkoa Songea walikwenda eneo la tukio na kufanikiwa kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu na hakuwa na jerhaa sehemu yeyote ya mwili na kwamba chanzo cha kujinyonga mpaka sasa hakijafahamika na hakuna ujumbe wowote aliouacha marehemu.

MWISHO.

No comments:

Post a Comment