About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, August 28, 2011

AFYA ZA WAFANYABIASHARA SOKO KUU SONGEA ZIPO HATARINI KWA KUKUBWA NA MAGONJWA YA MLIPUKO


                                           Na Gideon Mwakanosya,Songea.
WAFANYABIASHARA katika Soko kuu katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoa wa Ruvuma wapo katika hatari kubwa ya kukumbwa na magonjwa ya milipuko kikiwemo Kipindupindu kutokana na miundo mbinu ya maji taka yanayo simamiwa na mamlaka ya Maji safi na Maji taka Songea (SOUWASA) kuwa mibovu pamoja na wauzaji wa  nyama ya ng’ombe kwenye mabucha kutiririsha maji machafu wanayosafishia utumbo wa ng’ombe hadi maeneo wanayouzia nyanya,vitunguu na mbogamboga wafanyabiashara wadogo.
Mwandishi wa mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ jana alifanya mazungumzo na baadhi ya wafanyabiashara sokoni hapo ambapo walieleza kuwa miundo mbinu ya maji taka imekuwa ikipasuka na kutiririsha maji kwenye maeneo wanayouzia bidhaa zao na kusababisha adha kubwa kwa wafanyabiashara hao ambao wamekuwa wakilazimika kufanya kazi katika mazingira magumu.
Walisema katika hali ya kushangaza  soko hilo lina maafisa afya ambao wamekuwa wakifanya kazi kila siku kwenye eneo hilo ambalo lina mazingira machafu lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa.
Issa Hussen ambaye ni mfanya biashara katika soko hilo alieleza kuwa wafanyabiashara wa mbogamboga ambao wamekuwa wakitandika magunia chini kisha kuweka bidhaa zao kama nyanya, vitunguu wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu kwani kwenye maeneo wanayofanyia biashara hiyo maji yanayotiririshwa toka kwenye ma bucha ya nyama za ng’ombe wanayooshea utumbo wa ng’ombe pamoja na maji taka ambayo yanayo tiririka toka kwenye mtandao wa Souwasa yamekuwa yakipita kwenye eneo hilo wanayofanyia biashara na kuwaletea adha kubwa kwani wanunuzi wamekuwa wakikataa kununua bidhaa zao kutokana na maji machafu kuwa jirani na biashara zao.
 Kwa upande wake Afisa masoko wa Halmashauri ya Manispaa hiyo Salum Homera alipoulizwa na mtandao huu kuhusiana na malalamiko ya wafanyabiashara kuhusiana na kukithiri kwa uchafu kwenye soko kuu ambalo limekuwa likitiririsha maji machafu kwenye ambayo yamekuwa yakipita jirani kabisa na maeneo ya biashara zao alikiri kuwepo kwa tatizo hilo lakini alisema kuwa tatizo hilo lipo juu ya uwezo wake.
Homera alisema kuwa Ofisi yake ilisha toa taarifa kwa idara ya Afya na kwamba maafisa afya ndiyo walitakiwa kuona umuhimu wa kudhibiti hali hiyo iliyojitokeza sokoni na kwamba mamlaka ya maji safi na maji taka songea (SOUWASA) nao walishapewa taarifa na waliahidi kufika kufanyia matengenezo mtandao wa maji taka.
 Kwa upande wake Afisa afya wa Halmashauri ya Manispaa hiyo Mahundi alipohojiwa na nipashe kuhusiana na kukithiri kwa uchafu katika soko hilo, alieleza kuwa tatizo hilo Ofisi yake ilikuwa bado haijalipata lakini Afisa masoko ndiye alitakiwa kutoa taaarifa ki maandishi kwenye ofisi ya idara ya afya ili tatizo hilo liweze kufanyiwa kazi kirahisi kwani yeye ndiye msimamizi mkuu wa masoko yote ya halamashauri.
 Jitihada za mtandao huu za kumpata Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na maji taka (SOUWASA) Fransis Kapongo ziligonga mwamba baada ya kumpigia simu yake ya mkononi zaidi ya mara tatu bila kupatikana na nipashe ilifanya jitihada zaidi ya kuwasiliana na kaimu katibu tawala wa mkoa wa Ruvuma Dr.Anselmo Tarimo na kumuuliza juu ya uchafu uliokithiri sokoni Songea amabye alikiri na kudai kuwa tatizo hilo linalazimika kufanyiwa utaratibu wa haraka ili kulimaliza kuanzia mwanzoni mwa wiki hii ambapo wataalamu wote wa afya watalazimishwa wawepo kwenye soko hilo ili waone ni jins gani wataweka mazingira mazuri sokoni hapo ambayo yatawafanya wafanyabiashar wasikumbwe na magonjwa ya milipuko.

No comments:

Post a Comment