About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, August 26, 2011

Aliyekuwa Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Ally Said Manya


MADIWANI NANE WA CCM KUCHUANA KUGOMBEA UMEYA SONGEA
Na Stephano Mango,Songea.
CHAMA cha Mapinduzi (CCM ) Wilaya ya Songea mjini Mkoa wa Ruvuma kimeanza mchakato wa uchaguzi wa kura za maoni kujaza nafasi ya aliyekuwa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Ally Said Manya aliyefariki dunia kwa ugonjwa wa kisukari Julai 29 mwaka huu katika Hospitali ya Misheni ya Peramiho iliyopo wilaya ya Songea vijijini ambapo madiwani wanane na mgombea mmoja binafsi wamechukuwa fomu ya kuwania nafasi hiyo.
Akizungumza na mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ jana ofisini kwake Katibu wa CCM wilaya ya Songea mjini  Alfonsi Siwale alisema kuwa wagombea wa kiti cha Umeya kupitia CCM tayari wamechukua  fomu na kuzirudisha ofisini hapo mapema jana majira ya saa 10.30 jioni.
Siwale amewataja Madiwani waliojitokeza kuchukuwa za kuwania nafasi hiyo kuwa ni  Charles Mhagama diwani wa kata ya matogoro,Merius Ponera Diwani wa kata ya Tanga, Jemes Makene diwani wa kata ya Matarawe, Victor Ngongi diwani wa kata ya Ruvuma,Faustin Mhagama diwani wa kata ya Mshangano, Mariam Dizumba diwani viti maalumu, Genrida Haule diwani viti maalum, Christian Matembo diwani wa kata ya Seedfam pamoja na Willy kayombo ambaye ni Mwenyekiti wa jumuia ya wazazi Mkoa wa Ruvuma ambaye ndiye mgombea pekee binafsi aliyejitokeza kugombea nafasi hiyo.
Alisema kuwa ofisi yake ilipata barua toka kwa Mkurugenzi wa Manispaa hiyo ya kumtaka aanze mchakato wa kumuandaa mgombea kwa nafasi ya umeya kupitia CCM na chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) ambacho kinamadiwani kwenye halmashauri hiyo kwa lengo la kutaka kujaza nafasi ya meya ambayo iliachwa wazi baada ya Manya kufariki dunia.
Alieleza zaidi kuwa kwa sasa chama cha CCM wilayani humo kimepokea majina nane ya madiwani pamoja na mgombea mmoja binafsi ambao wote wamerudisha fomu za kutaka kugombea nafasi hiyo na baada ya hapo majina yatapendekezwa katika vikao mbalimbali vya chama wilaya na mkoani na kutoa maoni kwa kamati kuu ya CCM Taifa ambayo ndio itakayofanya uteuzi wa mwisho na kurudisha majina ambayo ndio yatapaswa kupigiwa kura na madiwani ndani ya baraza la madiwani wa CCM.
Siwale alifafanuwa kuwa baada ya madiwani hao kumpata mgombea ndipo jina la mshindi litapelekwa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa hiyo ambaye ndie atakayepanga tarehe ya uchaguzi wa kujaza nafasi hiyo kwa kumkutanisha na mgombea mwingine wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) endapo nao watampendekeza mgombea.
Ally Manya alikuwa diwani wa kata ya Lizaboni na alichaguliwa kuwa Mstahiki Meya wa Halmashauri hiyo Novemba mwaka jana na alifariki dunia baada ya kuuguwa kwa muda mrefu ugonjwa wa kisukari.
 MWISHO.

No comments:

Post a Comment