About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, August 30, 2011

KAMPUNI YA SONGEA NETWORK YAPANIA MAKUBWA KATIKA KILIMO NA ELIMU


                                     Na Thomas Lipuka,Songea
KAMPUNI ya Songea Network Centre na Valongo Network Centre za Mkoani Ruvuma zimeazimia kuimarisha kilimo cha Kahawa,ulezi na Jetropa katika Mkoa wa Ruvuma ili kuwakomboa wananchi wa kipato cha chini kwa kilimo hicho.
Kampuni hizo zimetambulishwa jana rasmi mbele ya Serikali ya Mkoa na kutaja malengo yao katika kuendeleza mazao hayo matatu kwa ustawi wa jamii za watanzania ambao zaidi ya asilimia 80 wanategemea kilimo.
Mkurugenzi wa Kampuni hizo Xaveri Kazimoto Komba ameyataja malengo yao kuwa ni kuendeleza elimu katika Mkoa,kuimarisha kilimo cha ulezi,kahawa na Jetropa,kukuza utamaduni na kuimarisha hali ya Mkoa kwa mazingira ili uoto wa asili usitoweke.
Komba alisema katika kuimarisha kilimo cha kahawa Mkoani Ruvuma tayari ameisha unganisha Mkoa na watafiti wa zao hilo toka Ujerumani ambao kwa kutumia teknolojia za kisasa wataliendeleza zao hilo na kuleta uzalishaji wenye tija ili kukuza kipato cha wakulima wa kahawa Mkoani Ruvuma.
Akiongelea hatua zingine za kuboresha uzalishaji wa zao hilo na mazao mengine yaliyo tajwa amesema hapata kuwepo na tatizo la soko kwani utaratibu umeisha andaliwa wa kununua mazao hayo iwapo yatazalishwa kwa kasi na kutunza ubora wake na soko limeandaliwa.
Akitambulisha mradi wa kuboresha elimu Kazimoto amesema tayari wameisha anzisha Sekondari ya St.Sapiensia ambayo ina kidato cha nne sasa na kuchukua wanafunzi wa dini zote wa kike na wa kiume,shule ambayo iko Parokia ya Mjimwema manispaa ya Songea.
Katika hatua nyingine tayari Songea Network Centre imeisha panda miti zaidi ya 500 ya kivuli matunda na mbao kwa hatua ya kulinda na kuboresha mazingira,miti ambayo imepandwa Songea mjini na Kijiji cha Mbinga Mhalule Tarafa ya Muhukuru.
Naye Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Vestina Nguruse ambaye kwa cheo chake ni mshauri wa mipango Mkoa amesema mradi wa kilimo kinachojali watu unaoanzishwa na Songea Network Centre uwe endelevu kwa kuwa mipango yake ni ukombozi kwa watu wa Ruvuma.
Amesema shida kubwa ni soko kwa mazao ya wakulima na bei zisizo za uhakika ambazo hubadilishwa mara kwa mara kutokana na soko la dunia linavyoendelea lakini kutokana na utafiti wa kina uliofanywa na Songea Network Centre bila wasiwasi suala la soko litadhibitiwa kikamilifu.
Nguruse amefafanua kuwa fursa za kuendeleza mazao haya katika Mkoa zipo za kutosha akataja uwepo wa ardhi safi kwa kilimo cha kahawa,ulezi na Jetropa  ni nguvu kazi ya kutosha yaani wakulima uwepo wa Bandari ya Mtwara na ujenzi wa barabara inayoendelea toka Mtwara Mbamba bay pia mito na mabonde yenye maji wakati wote kwa kilimo cha umwagiliaji.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa Nguruse aliwaasa viongozi wa mradi kusimamia mradi huo uwe endelevu na utimize azima yake ya kumkomboa mkulima wa Mkoa wa Ruvuma
Wakati huo huo imefahamika kuwa jitihada za kupata soko la uhakika kwa mazao hayo matatu zimeletwa na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Ahamad Ngemara ambaye amefanya jitihada kubwa kwa suala la masoko nchini Ujerumani.

1 comment:

  1. Menejimenti ya Tanexa (www.tanexa.com) iwasiliane na kampuni zilizotajwa pamoja na balozi wa Tanzania nchini Ujerumani ili uwepo uwezeshaji makini katika malengo na matarajio husika.

    ReplyDelete