About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, September 5, 2011

ASAKWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA DADA YAKE

                                        Na Gideon Mwakanosya,Songea.
 
JESHI la Polisi mkoani Ruvuma linamsaka Rashuel Mapunda mkazi wa mtaa wa misheni Mbinga mjini kwa tuhuma za kumbaka dada yake mwenye umri wa miaka 14  ambaye jina lake limeifadhiwa anayesoma kidato cha kwanza katika shule ya sekondari ya kutwa ya Makita.
 
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 9.alasali nyumbani kwa wazazi wao ambako inadaiwa Mapunda alimkamata dada yake kwa nguvu na kumfanyia kitendo cha unyama.
 
Kamuhanda alifafanuwa zaidi kuwa inadaiwa kuwa siku ya tukio msichana huyo akiwa anajiandaa kufanya shughuli za usafi nyumbani kwao ghafla alimkuta kaka yake amefika na kumkamata na kumalazimisha avue nguo kasha alifanya nae mapenzi.
 
Alisema kuwa wakati Mapunda anafanya tendo hilo la kinyama kwa dada ake ambaye alipiga kelele kwa ishara ya kuomba msaada majirani wasikia na walipofika kwenye nyumba hiyo walimkuta mapunda tayari ameshambaka msichana huyo.
 
Kamuhanda alisema kuwa majirani pamoja na wazazi wake wakiwa kwenye eneo la tukio walianza kumkimbiza Mapunda kwa lengo la kutaka kumkamata walishindwa baada ya yeye kuwatoroka a kutokomea kusikojulikana.
 
Alisema kuwa baadae msichana huyo walimpeleka kwenye hospitali ya wilaya ya Mbinga kwa matibabu ambako ilibainika kuwa mwanafunzi huyo ameumizwa vibaya sehemu zake za siri ambazo zimeonekana kuwa na michubuko mingi.
 
Kamanda alisema kuwa jeshilake linaendelea kumsaka mtuhumiwa huyo na kwamba akipatikana atafikishwa mahakamani kujibu shitaka linalomkabili.
 
MWISHO.  

No comments:

Post a Comment