About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, September 6, 2011

TGNP NA HARAKATI ZA UKOMBOZI KWA WANAWAKE NCHINI

 

Na Juma Nyumayo, Dar es Salaam
WANAWAKE nchini wameshauriwa kuziangalia changamoto juu a uelewa wa masuala ya uchumi na ukombozi wa wanawake baada ya miaka 50 toka uhuru ambapo wanawake wengi waeachwa nyuma kielimu na kiuchumi.
Hayo yameelezwa leo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Jinsia ya TGNP, Diana Mwiru, wakati wa Ufunguzi wa Warsha ya Uelewa wa Masuala ya uchumi na wanawake yanayoshirikisha viongozi mbalimbali wakiwemo madiwani toka mikoa yote ya Tanzaia Bara.
Mwiru, amesema, katika miaka 50 iliyopita wanawake wa nchi hii wameendelea kuachwa nyuma katika kumiliki na utoaji wa maamuzi juu ya rasilimali.
Mkuu huyo, amebainisha kuwa wakati umefika hivi sasa kwa jamii ya kitanzania kuhakikisha maisha bora kwa kila mtanzania yaapatikana kwa kuwashirikisha watu wote kutafuta na kutumia rasilimali za taifa.
Aemesema ni muhimu wa serikali zetu kuhakikisha wananchi hasa wanawake wanashiriki katika mchakato wa bajeti na iwe na mtazamo wa kijinsia.ngi wao ni viongozi wa Dini, waheshimiwa Madiwani, Viongozi wa asasi zisizo za iserikali waandishi wa Haari na wanaharakati wanawajibu wa kuhakikisha uchumi na ukomboziwa mwanamke kimapinduzi unakwenda sambama na elimuya mtoto wa kike.
Mwateba amesema mia na desturi ambazo ni vikwazo katika ukombozi huo a faa zibainishwe wazi na kwama zijengwe nguvu za pamoja katika kutetea haki za uchumi.
Katika hali nyingine washiriki wawarsha hiyo wameeleza kwa kuna mabadiliko mengi yanajitokeza hivi sasa na kwamba baadhi ya Sera na kanuni zinawakandamza wanawake katika harakati za kumkomboa
Prisca Haule, Mheshimiwa Diwani Viti Maalum halmashauri ya Mbinga alisema inashangaza kuona Diwani wa Viti maalum hana nafas kugombea uongozi wa juu kama Uenyekiti wa Halmashauri au Umeya wa Manispaa.
"Hizi sera zinatunyanasa na kutuweka nyuma a kuwa wanyonge, alisema Haule.
Kauli hiyo iliungwa Mkono na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Morogoro Vijijini Kibena Kingo kuwa hata wabunge viti Maalumu nao hawawezi kuteuliwa kupata nafasi ya Uspika au Uwaziri Mkuu.
"Hawawezi kupata nafasi kama hizo hivyo ukombozi wa mwanamke unavikwazo vingi," alisema Kingo.
Wakati vikwaz hivyo vikibainishwa, Diwani Anna Lyimo kutoka Halmashauri ya Moshi amewalalamikia wanaume wa Moshi kuwaingilia wanawake katika zao lao la Ndizi ambalo kimsingi ni zao la chakula na likimilikiwa na wanawake.
Lyimo alisema kuingiliwa huko kumetokana na kuanguka kwa zao la Kahawa na kitendo hicho kinaibua mgogoro wa kimaslahi ya kiuchumi.
Naye mwezeshaji Rehema Mwateba, alisema kuna mifumo ya kiuchumi na Matabaka ambayo bado yanamkandamiza mwanamke na hivyo washiriki ambao we
Mafunzo hayo ya siku tano yanaendelea katika Ukumbi wa Kitivo cha Uhandisi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo washiriki wanategemewa kujenga uelewa wa masuala ya uchumi na ukombozi wa waawake kimapinduzi na kuwaelewesha watoa maauzi katika maeno yao wanayotoka.
Mwisho

No comments:

Post a Comment