About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, September 19, 2011

WANAHARAKATI WAITAKA SERIKALI KUREKEBISHA SERA NA SHERIA KANDAMIZI

                                                        Na Stephano Mango
WANAHARAKATI wameshauri sera  na sheria  mbalimbali zilizotungwa na zitakazotungwa  kwa ajili ya kukuza uchumi ili kuleta maisha bora endelevu kwa  wananchi nchini  zifanyiwe ufatiliaji ili kuhakisha zinawanufaisha watoto na wasichana wanaofanya ajira  za ndani .
Wakichangia mada katika warsha ya Mapambano ya wanaharakati kwa wanawake katika njia za kujiajiri,kupata ajira na kujiletea maisha endelevu katika Tamasha la 10 la wiki ya Jinsia lililo malizika juzi jijini Dar es salaam wanaharakati hao  walisema sheria nyingi zimetungwa na zimelenga  kuleta maisha bora kwa watanzania wakiwemo wanawake  lakini hakuna  ufatiliaji unaofanyika kuhakikisha zinatekelezwa ili kuwanufaisha  katika masuala ya kupata ajira.
Mwenyekiti wa Mtandao wa Jinsia Tanzania,Mary Rusimbi alisema ili kuondokana na matatizo ya ajira kwa wanawake ni vizuri  sera za kitaifa za kuondokana na umaskini zikiwemo sera ya ajira zitekelewe.
“Sera hizi inabidi zifanyiwe ufatiliaji ili kutambua kasi ya utekelezaji katika kuleta maisha bora na endelevu kwa wananchi,elimu katika masuala ya ajira inabidi itolewe ili mfanyakazi  akiwemo wa nyumbani  aweze kujua haki na wajibu wake katika kazi hizo”alisema Rusimbi.
Na kufafanua kuwa  elimu hiyo itampa mwongozo kutambua kazi za nyumbani anazopaswa kufanya na sizopaswa kufanya.
Alieleza kuwa haki mojawapo ambayo mfanyakazi wa ndani anapaswa kuidai ni kutambulika katika chama cha wafanyakazi nchini.
Wanaharakati hao walieleza kuwa wasichana wanaofanya kazi za ndani wanaishi katika mazingira magumu na hii ni kutokana na kunyimwa fursa za kushiriki katika mijadala,kupata elimu na kufanya maamuzi.
Naye Ruth meena akizungumza katika warsha alisema kuwa ili kuondoa tatizo hilo basi sera za elimu ziboreshwea ili kuwawezesha wafanyakazi wa ndani kufahamu haki zao za ajira na kujipatia maisha endelevu.
Lakini pia alitoa wito kama mtoto wa kike amefeli mtihani wa shule ya msingi si vizuri akiozeshwa au kulazimishwa kufanya kazi za ndani  badala yake apelekwe shule za ufundi stadi ili baadae aweze kujikomboa kiuchumi.
Andrew Njau kutoka Kilimanjaro, wilaya ya Hai alisema elimu endelevu kwa vijana ni suluhisho pekee la kupambana na tatizo la ajira na umaskini nchini hivyo basi  serikali inatakiwa kuwajibika kuanzia ngazi za chini kuhakikisha utekeleaji wa sera hizo unatiliwa mkazo.
Kwa upande wake Veronica Ngweya ,kutoka Msumbiji alisema ili kutatua tatizo la ajira kwa wasichana wa ndani serikali  yao imeanzisha kampeni maalum ya kuwafikia na kukusanya maoni ili kutambua matatizo wanayaokumbana nayo na kisha kuwapatia elimu.
“Tunawafundisha sera zitakazowajengea uwezo wa kujitambua na kuzipigania hali zao pale wanapoona zimekiukwa”alisema Ngwenya.
mwisho

No comments:

Post a Comment