About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, September 13, 2011

WANAHARAKATI WAZIKEMEA SERIKALI ZA AFRIKA KWA UKANDAMIZAJI

 Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP)  Ussu Mallya akielezea tamasha la jinsia 2011 linaloendelea kufanyika jijini Dar Es Salaam
 Waandishi wa habari wakiwa kwenye moja ya vikao kwa ajili ya maandalizi ya kulipoti habari mbalimbali
 Wanaharakati mbalimbali wakiwa wanafuatilia mada zinazowasilishwa na wadau mbalimbali wa haki za binadamu
 Wanahabari mbalimbali kutoka katika vyombo tofauti tofauti wakiendelea kuchapa kazi wakati wa tamasha la jinsia 2011 linaloendelea kufanyika katika viwanja vya TGNP Jijini Dar Es Salaam
 Kikundi cha ngoma ya asili kikitumbuiza wakati wa tamasha
 Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari wanawake nchini Ananilea Nkya akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mtandao wa jinsia tanzania TGNP ikiwa ni maandalizi ya kuhabarisha umma
WANAHARAKATI WAZIKEMEA SERIKALI ZA AFRIKA KWA UKANDAMIZAJI
 Na Stephano Mango,Dar Es Salaam
WANAHARAKATI nchini wamezitaka Serikali  za nchi barani Afrika, kuhakikisha rasilimali zinawanufaisha wananchi hususani wanawake na watoto wanaoishi pembezoni ili kuweza kupunguza matabaka ya wenye nacho na wasio kuwa nacho ili kuweza kujenga jamii iliyostaarabika

Mwanaharakati wa masuala ya ardhi nchini Ghana, Profesa Dzodzi Tsilsata, alisema jana alipokuwa akifungua Tamasha la Jinsia, linalofanyika katika viwanja vya TGNP, Jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Tsilsata, miaka michache iliyopita kumekuwepo na ongezeko kubwa kati ya wenye nacho na wasinacho hali inayosababisha kuwepo na matukio mengi ya uvunjifu wa amani, kwa kuandamana, kugoma ama vurugu mbalimbali.

Alisema, Serikali badala ya kupunguza hali hiyo imekuwa ikizembea kuchukua hatua stahiki na badala yake inawaongezea makali ya maisha wananchi wake kwa kuwaachia viongozi wake wakifanya vitendo viovu vya ubadhilifu wa rasilimali za taifa.

Alisema kuwa, Afrika inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya kukubali sera mbovu kutoka katika mataifa ya magharibi na taasisi za fedha za kimataifa ambazo zimekuwa zikiwakandamiza wananchi wengi.

Naye Mwenyekiti wa tamasha hilo, Mary Rusimbi alisema kuwa Serikali za Afrika zimekuwa zikishindwa kutengeneza sera stahiki kwa wananchi wake na kupelekea hisia za kuwa na ukoloni mamboleo

Rusimbi alieleza kuwa Tanzania imetimiza miaka 50 baada ya uhuru lakini bado haijaweza kujitegemea kiuchumi,kisiasa,kidini,kijamii,kijeshi na kiutamaduni kwani imekuwa ikitawaliwa na utegemezi mkubwa kwa nchi za magharibi kupitia makampuni makubwa ya kimataifa ya uwekezaji
.
Alisema kuwa Serikali hutekeleza kwa niaba ya nchi za magharibi sera za utandawazi kupitia sera za ulegezaji wa uchumi na uuzaji wa bidhaa nje ili kuweka mazingira wezeshi kwa makampuni ya kibepari badala ya wazalishaji wadogowadogo

Alieleza kuwa matokeo yake mapato ya serikali yanazidi kutegemea makampuni machache yanayouza nje bidhaa kama vile madini,mbogamboga , maua,utalii na viwanda ambapo wanawake ndio wamekuwa waathirika wakubwa wa mifumo ya unyonyaji

Alifafanua zaidi kuwa kutokana na hali hiyo wanawake wengi waliopo pembezoni wamekuwa wakinyang’anywa rasilimali zao na kupewa watu wenye nguvu ya kiuchumi kutokana na mwingiliano wa mifumo kandamizi ya kibeberu na kibepari na mfumo dume unaowaacha wanawake wengi wakiwa mikono mitupu
mwisho

No comments:

Post a Comment