About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, September 13, 2011

MENEJA WA SHIRIKA LA POSTA RUVUMA ADAIWA KUWANYANYASA WAFANYA KAZI WAKE

                                               Na Gideon Mwakanosya,Songea.

WAFANYAKAZI wa shirika la Posta Tanzania mkoani Ruvuma wameulalamikia uongozi wa shirika hilo mkoani humo kwa vitendo vya unyanyasaji kwa wafanyakazi likiwemo cha wafanyakazi wawili kusimamishwa na kufukuzwa kazi kwa madai kuwa wameiba fedha kiasi cha sh.10,620 mali ya shirika hilo.

Wafanyakazi hao ambao walitoa malalamiko yao kwa masharti ya kutotajwa majina kwa kuhofia ajira zao walisema kuwa unyanyasaji uliopo katika shirika hilo unaofanywa na Meneja wa Shirika hilo mkoani Ruvuma Rochus Assenga unawafanya wawe wanafanya kazi kwa hofu kubwa.

Walisema kuwa kitendo cha kuwasimamisha wafanyakazi wenzao na mmoja kumwachisha kazi kinaonesha wazi ukiukwaji wa haki za wafanyakazi kwani wafanyakazi hao mpaka sasa hakuna kosa lolote la msingi linaloweza kuwafanya wasimamishwe au kuachishwa kazi.

Mfanyakazi aliyesimamishwa kazi ametajwa kwa jina la Johnson Miyola na aliyeachishwa kazi Peter Sendama ambaye mpaka sasa barua ya kuachishwa kazi ajakabidhiwa ingawa amepewa taarifa hiyo ya kuachishwa kazi na meneja kwa mdomo na kutakiwa asiingie kwenye ofisi za shirika hilo wakati uongozi unamuandalia barua pamoja na mafao ya kuachishwa kazi.

Uchunguzi uliofanywa na waandishi wa habari umebaini kuwa licha ya kuwasimamisha kazi  na kumwachisha  mmoja tayari wafanyakazi hao walishapelekwa polisi na kufunguliwa kesi ya wizi namba SO\ IR\3962\2011 katika kituo kikuu cha Songea tangu Agosti 19 mwaka huu.

Mfanyakazi mmoja aliyeachishwa kazi Sendama alipoulizwa na waandishi wa habari amekiri kuchishwa kazi kwa mdomo na kwamba barua ya kuachishwa kazi pamoja na mafao atapewa siku ya Ijumaa kwa mujibu wa maelezo aliyoyatoa meneja wa shirika hilo Assenga

Alisema ameshangazwa kuona atua kali zikichukuliwa dhidi yake ambapo awali tangu aanze kazi kwenye shirika hilo hajawi kupewa barua ya onyo au kalipio kali kabla mfanyakazi hajaachishwa kazi.

“ Sina kosa jingine ambalo meneja alishanionya mara tatu kwa kujaza fomu tatu ambazo mfanyakazi kabla hajaachishwa hujazwa na kabla ya hapo meneja hajawahi kunipa onyo wala fedha hizo anazodai nimeiba si kweli bali kulikuwa na tatizo la kiufundi lililojitokeza kwenye mtandao na kusababisha kumwandikia mteja risiti kwa mkono.”alisema Bw. Sendama.

Hata hivyo baadhi ya wafanyakazi wa shirika hilo tawi la Songea wameeleza kuwa tangu meneja huyo Assenga afike Mkoa wa Ruvuma baada ya meneja aliyekuwepo kustaafu amekuwa na tabia ya kuwanyanyasa na kudai kuwa yeye amuogopi mtu wa aina yeyote kwani ametokea makao makuu ya shirika hilo na kwamba Posta masta mkuu ni swaiba wake hivyo hawezi kumfanya kitu chochote na ni lazima amsikilize anachosema.

Naye Meneja wa shirika hilo mkoani Ruvuma  Assenga alipofuatwa na waandishi wa habari ofisini kwake kutaka atoe ufafanuzi juu ya malalamiko dhidi yake alidai kuwa yeye sio msemaji wa shirika na kuwataka waandishi wamtafute posta masta mkuu wa shirika hilo ndio msemaji na baadae alipoona waandishi wa habari wanaendelea kumuliza maswali aliondoka ofisini kwake na kuwaacha waandishi wa habari wakiduwaa kwenye jengo la shirika hilo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi wa shirika la posta Tanzania tawi la Songea Gisla Mhagama alipotafutwa na  waandishi wa habari ili ataoe ufafanuzi juu ya malalamiko ya wafanyakazi dhidi ya uongozi hakuweza kupatikana kwa njia ya simu kwa kuwa yuko safarini nje ya Mkoa.

Hata hivyo waandishi wa habari waliwatafuta viongozi wa chama hicho (COTWU) kanda ya Mbeya kwa njia ya simu ambapo walifanikiwa kumpata katibu wa chama hicho  Getrud Mlai na mwenyekiti wake Peter Songela walishangazwa kusikia kuwa wafanyakazi wa tawi la Songea wamekuwa na malalamiko mazito dhidi ya uongozi na walidai kuwa wao bado hawajapata malalamiko rasmi lakini wanafanya taratibu za kwenda Songea kwenda kusikiliza kilio cha wafanyakazi wiki ijayo.

Akizungumza kwa njia ya simu Posta masta mkuu wa shirika la Posta Tanzania Deos Mndeme alieleza kuwa ni kweli ofisi yake inataarifa kuwa kunawafanyakazi wawili wa shirika hilo ambao walipelekwa polisi wakituhumiwa kuwa ni wezi wameiba fedha sh.10,620 lakini hana taarifa ya aina yeyote kama wafanyakazi hao wamesimamishwa na kuachishwa kazi kwani maswala ya utawala yanamgawanyo na mambo ya utawala wa mikoani yanaishia mikoani yeye anashughulikia mambo makubwa.

Aidha mndemi alikanusha kauli ya meneja wa shirika hilo mkoani Ruvuma Assenga ya kusema kuwa yeye yuko jirani naye na ni swaiba yake jambo ambalo alidai kuwa linaleta mazingira ya kumchafua kwani yeye ni mtawala wa shirika na wafanyakzi wote bila kuwa na ubaguzi labda uhusianao huo katika yangu na yeye anaujuwa yeye na si vinginevyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma  Michael Kamuhanda alipoulizwa na waandishi wa habarí kuhusiana na wafanyakazi wawili wa shirika la posta kukamatwa na kuwekwa mahabusu kwa tuhuma za wizi wa sh. 10,620 za shirika hilo amekiri kushikiriwa kwa wafanyakzi hao lakini ameeleza kuwa jambo hilo liko kwenye upelelezi na bado halijathibitishwa kama wafanyakazi hao kama waliiba au la.

MWISHO.

No comments:

Post a Comment