About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, October 4, 2011

BUNGE LATAKIWA KUHAKIKISHA SUALA LA PENSHENI KWA WAZEE LINAINGIZWA KWENYE BAJETI YA TAIFA

  Mzee huyu ni miongoni mwa watu wanaotakiwa kupewa matibabu bure na pensheni nchini ili aweze kujikimu na maisha yake

Na Augusino Chindiye, Tunduru
BUNGE la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania limeahidi kusimamia na kuhakikisha kuwa mpango wa kuanza kuwalipa pensheni  wazee hapa nchini unaingizwa katika Bajeti ya Bunge lijalo na kuanza kulipwa mapema 2012.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru  Juma Madaha akiwa ananukuu Hotuba iliyokuwa imeandaliwa na Mwenyekiti wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  Jenista Mhagama ambaye alitakiwa kuwa mgeni Rasmi katika maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani iliyofanyika katika viwanja vya Baraza la Iddi Mjini Tunduru.

Akifafanua taarifa hiyo Dc,Madaha alisema kuwa Mhagama kwa kushirikiana na Wabunge wenzake wakiwemo wabunge kutoka Mkoa wa Ruvuma ameahidi kutoa msukumo mkubwa na kuhakikisha kuwa mswada wa kuanza kuwalipa Pensheni unatungiwa sheria mapema iwezekanavyo ili wazee wa Tanzania waanze kunufaika na mafao hayo.

Hotuba hiyo iliendelea kueleza kuwa wakati Wabunge hao wakishughulikia tatizo hilo tayari Serikali imeanza kuweka msukumo wa kuendelea kuwahudumia Wazee kote nchini waanze kupata huduma za Matibabu bure kupitia mkakati wa kuwaagiza Waganga wakuu wa Hospitali zote nchini kutenga vyumba maalumu vya kutolea huduma hiyo kwa wazee zikiwa ni juhudi za kuwaondolea kero na foleni.

Alisema Sambamba na kuwepo kwa zoezi hilo pia Hotuba hiyo ilieleza kuwa tayari Serikali pia kupitia Wakuu wa Wilaya kote nchini wamewaagiza watenzaji wa Vijiji kutekeleza agizo la kuwaandikia Wazee barua zitakazo wafanya watambuliwe na kuanza kupatiwa huduma za matibabu bure kuanzia ngazi za Zahanati,Vituo vya afya na Hospitali.

Awali akisoma Risala ya Wazee katika madhimisho hayo Katibu wa Chama cha Wazee wa Wilaya ya Tunduru (HAWATU) Jafari Msonjele alisema kuwa pamoja na kundi hilo kukabiliwa na changamoto nyingi za kimaisha Wazee wengi kote nchini wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya kulea kundi kubwa la Watoto yatima ambao wengi wao wameachwa na ndugu,jamaa na Watoto wao waliopoteza maisha kutokana na ugonjwa wa Ukimwi.

Wazee hao pia katika taarifa yao wakagusia changamoto kubwa ya kitaifa inayo wakabiri wazee wenzao wastaafu ambao wamekuwa wakiyumbishwa kwa muda mrefu kulipwa pensheni zao na mashirika ya PPF,PSPF, na LPF na wakatumia nafasi hiyo kuyaomba mashirika hayo kuridhia maombi ya wanachama wake ya kuanza kuwalipa wanachama wake malipo ya mwezi mmoja, Mitatu na Sita bila kupitisha muda wake pamoja na kuangalia uwezekano wa kama kuna nyongeza basi iongezwe kwa wanachama wote  ili kuwapunguzia makali ya maisha.

Nae Mwenyekiti wa Chama hicho Said Kabora akitoa neno la shukurani wakati wa kufunga maadhimisho hayo pamoja na kulipongeza Bunge kwa kauli hiyo alisema kuwa Wazee bado wanayo imani na serikali yao na wana amini kuwa macho hayo yaliyo ahidiwa kwa vipofu na chombo kinacho wawakilisha katika utoaji wa maamuzi yatatekelezeka na kuwafanya wazee kote nchini kufurahia matunda ya nchi yao. 
  Mwisho

No comments:

Post a Comment