About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, October 25, 2011

UCHAKACHUAJI WA MAPATO YATOKANAYO NA MAZAO YA MISITU MBINGA WASABABISHA HASARA

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Shaib Mnunduma
Na Gideon Mwakanosya,Mbinga
HALMASHAURI ya Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma imepata hasara ya shilingi milioni 18 kupitia idara yake ya maliasili na mazingira kutokana na uzembe uliofanywa na watumishi wachache wa idara hiyo, waliopewa dhamana ya ukusanyaji wa ushuru wa mazao ya misitu.
Kwa mujibu wa vyanzo vya uhakika kutoka katika halmashauri hiyo ambavyo vilizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti kwa sharti la kutotaja majina yao, vilisema kuwa hasara hiyo imetokea kufuatia vitabu vyenye risiti ambavyo hutumika kukusanyia ushuru huo vimepotea katika mazingira ya kutatanisha.
Habari zinaeleza kuwa jitihada za kutafuta vitabu hivyo vilivyopotea mpaka sasa zimegonga mwamba jambo ambalo uongozi wa wilaya ya Mbinga, ulilazimika kuchukua hatua za kuripoti kituo kikuu cha polisi kwa msaada zaidi ambapo baadhi ya watumishi wa idara ya maliasili na mazingira wilayani humo waliwekwa mahabusu kwa siku kadhaa.
Aidha pamoja na watumishi hao kuwekwa mahabusu hivi sasa wameachiliwa huru na hakuna hatua zingine walizochukuliwa huku wakiendelea na kazi zao kama kawaida kitendo ambacho kimekuwa kikisababisha kuzua maswali mengi kutoka kwa watumishi wengine wa halmashauri hiyo.
Utaratibu wa halmashauri ya wilaya hiyo katika utoaji wa vitabu hivyo unaeleza kuwa alikabidhiwa mkuu wa kitengo cha kukusanya ushuru wa mazao ya misitu Nambole   Nanyanje ambaye huwagawia watumishi wenzake wanaohusika na suala la kukusanya ushuru huo.
Mwandishi wa habari hizi alipomuuliza kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mbinga Bernard Semwaiko juu ya tuhuma hizo alikiri kuwepo kwa upotevu wa fedha na vitabu hivyo huku akisema halmashauri yake imekwisha kamilisha utatuzi wa jambo hilo.
“Ni kweli kiasi hiki cha fedha kilipotea kutokana na upotevu wa vitabu vilivyokuwa vikitumika kukusanyia ushuru wa mazao ya misitu, najua umewahi kusikia kuna baadhi ya watumishi tuliwaweka mahabusu”, alisema Semwaiko.
 Kadhalika Mwandishi alipotaka kujua undani wa tatizo hilo Semwaiko alifafanua kuwa lilibainika kufuatia wakaguzi waliokuwa wakifanya kazi ya kukagua mahesabu ya halmashauri hiyo, ndipo wakaguzi hao waligundua kuna upotevu wa fedha hizo na vitabu, yenye jumla ya thamani ya shilingi milioni 18 kutoka idara ya maliasili na mazingira wilayani humo ambavyo vilitumika kukusanyia ushuru wa mazao ya misitu.

No comments:

Post a Comment