About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, November 14, 2011

MRADI WA UPIMAJI VIWANJA 18000 WAZINDURIWA KWA MBWEMBWE MBALIMBALI KATIKA ENEO LA BEROYA KATA YA MSHANGANO

 Mgeni Rasmi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati za Huduza za Uchumi na Jamii katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Genfrida Haule wa tatu toka kushoto ambaye alimwakilisha Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Charles Mhagama akizindua mradi wa upimaji wa viwanja 18000 katika eneo la kata ya Mshangano kwa kutumia Kampuni ya Ardhi Plan huku akishuhudiwa na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali
Mgeni rasmi Genfrida Haule akikagua barabara iliyochimbwa na wananchi wa Kta ya Mshangano ndani ya eneo la mradi wa upimaji wa viwanja huku akisindikizwa na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali katika Manispaa ya Songea
 Mgeni Rasmi Genfrida Haule akiwahutubia wananchi waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa mradi wa kisasa na wa aina yake wa upimaji wa viwanja 18000
 Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali wakisikiliza hotuba ya ufunguzi wa mradi wa upimaji wa viwanja iliyokuwa ikitolewa na mgeni rasmi Genfrida Haule
Sehemu ya barabara iliyochongwa na wananchi kwa kupata ujira wa kulipwa Tshs 5000 kwa kila mmoja kwenye eneo la mradi

MRADI WA UPIMAJI VIWANJA 18000 SONGEA KUWAKOMBOA WANANCHI KIUCHUMI
Na Stephano Mango,Songea
IMEDHIHIRIKA kuwa tatizo la makazi holela ambalo limeshamiri nchini limetokana na kutokuwa makini katika mipango miji na ukosefu wa wataalamu wa mipango miji wenye ubunifu na kusababisha adha kubwa kwa wananchi kutokana na wananchi kuvamia maeneo mengi na kujenga holela
Na kusababisha maeneo hayo  mengi ya aina hiyo kukosa miundombinu ya maji safi na maji taka,barabara na nishati ya umeme na kufanya mikakati mbalimbali ya maendeleo  kutofikiwa kikamilifu,jambo ambalo linawezekana kuepukwa ikiwa kila mtu atatimiza wajibu wake kwa kukomesha ujenzi wa makazi holela
Novemba  19 mwaka 2011 nilibahatika kuhudhuria uzinduzi wa mradi wa kisasa  na wa aina yake ambao haujawahi kutokea tangu nchi ipate uhuru wake mwaka 1961 wa upimaji wa viwanja 18,000 katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea
Mradi huo umezinduriwa katika kata ya Mshangano yenye mitaa  mitano ya Namanyigu,Mitendewawa,Mhumbezi,Chandarua na Mshangano yenye jumla ya kaya 1508 zenye wakazi 7540 ikiwa wanaume 3196 na wanawake 4344
Ambapo wakazi wa kata hiyo kama walivyo wakazi wa kata zingine 20 zilizopo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Songea wanajishughulisha na kilimo,ufugaji,na biashara ndogondogo katika  kujitafutia kipato cha maisha yao,
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa upimaji wa viwanja hivyo alikuwa Mshahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Charles Mhagama ambaye aliwakilishwa na Mwenyekiti wa Kamati za Huduma za Uchumi na Jamii wa Manispaa hiyo Genfrida Haule
Akizindua mradi huo wa upimaji viwanja hivyo  Haule alisema kuwa  Suala la upimaji viwanja ni hatua kubwa ya maendeleo kwa kuwa baada ya upimaji miundombinu ya maji na umeme itakuja na wananchi wameongeza kipato kwa kuweza kukopa  na kuendesha miradi kupitia viwanja  na nyumba zao huku viwanja vikipandishwa thamani
“Mradi huo utawainua kiuchumi wananchi wa Kata ya Mshangano kwa sababu wataweza kukopaa kupitia makazi yao  na kwamba wataweza kuishi katika makazi bora yaliyopimwa na kufanya mji wa Mshangano kuwa wa kisasa zaidi kuliko maeneo mengine ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea”alisema Haule
Akielezea historia ya Mradi huo Afisa Mtendaji wa Kata ya Mshangano Stan Kibiki alisema kuwa mradi huo wa upimaji wa viwanja kwa kutumia Kampuni uliibuliwa na wananchi wenyewe baada ya kuona wanakaa na kuishi katika makazi holela yasiyopimwa kwa muda mrefu
Kibiki alisema kuwa kwa muda wa miaka mingi wananchi wa kata hii wamekuwa wakipeleka maombi Halmashauri ya kuomba kupimiwa maeneo yao bila mafanikio kutokana na Halmashauri kukosa uwezo wa kifedha
“Mwaka 2010 kata yetu ilibahatika kupata mradi wa upimaji wa viwanja ilibahatika kupata mradi wa upimaji viwanja wa Halmashauri lakini bahati mbaya fedha yenyewe ilikuwa kidogo kwani waliweza  kupima viwanja 347 katika mtaa wa Namanyigu eneo dogo mashambani hivyo tatizo la wananchi kuishi katika makazi holela lilibaki palepale”alisema Kibiki
Alisema kuwa wananchi  kwa kushirikiana na viongozi wao katika kutatua tatizo hili waliamua kutafuta njia mbadala ambayo kwa kutumia sheria namba 8 ya Mipango Miji ya 2007 walitafuta Kampuni ya Ardhi Plan ya Jijini Dar Es Salaam ili iweze kuwapimia viwanja katika maeneo yao
Alieleza kuwa baada ya kuipata Kampuni hiyo makubaliano yakawa malipo ni ardhi kwa ardhi yaani wanapima ardhi wanalipwa ardhi kwa asilimia za kwamba mwananchi anapata 60% ya ardhi iliyopimwa na Kampuni inapata 40% ya ardhi iliyopimwa
Alifafanua kuwa asilimia 40% inayotolewa kwa Kampuni inatumika katika kuandaa michoro ya ubunifu wa mipango Miji (10%),kupima viwanja (10%)kuchonga barabara (10%) na faida ya Kampuni (10%) na kwamba mradi huu hauhusishi malipo ya fidia yoyote hii ni kwa makubaliano ya wananchi wenyewe na itakuwa kwa kusogezana
Afisa huyo alisema kuwa maeneo ya umma kama vile soko,shule,zahanati ,makaburi,stendi,msikiti,kanisa na maeneo ya wazi(open space)  yatatolewa bure katika mradi huo na kufanywa kuwa mradi wa kwanza kuibuliwa na wananchi wenyewe kwa kuitumia Kampuni ya Ardhi Plan kupanga mji wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea
Alieleza kuwa gharama za mradi huo zinatolewa na wananchi wenyewe kwa kutoa ardhi badala ya kusubiri  Serikali mpaka ipate uwezo wa kifedha ambapo kwa wale wenye maeneo madogo yaani kiwanja kimoja mpaka viwili wanatozwa gharama ya fedha shilingi laki moja(100,000/=) kwa kiwanja kimoja na laki mbili(200,000) kwa viwanja viwili kama gharama za upimaji
Kibiki alisema kuwa mitaa ambayo  michoro yake imekamilika ni Mshangano,Namanyigu, na Mitendewawa yenye jumla ya viwanja elfu kumi na nane (18,000/=) ambapo mitaa mingine itafuata baadaye
“Mchoro ambao tayari mawe yameshapandwa ni mchoro namba 9 ujulikanao kama Beroya na sasa wananchi wanaendelea na uchongaji wa barabara mchoro ambao una jumla ya viwanja 800”alisema Kibiki
Alisema kuwa mradi huo umesifiwa na viongozi wengi na wanaharakati mbalimbali wa masuala ya ardhi na maendeleo ya wananchi wanyonge kwani wamefanikiwa kupata maeneo yaliyopimwa na kuthaminiwa kwa ajili ya makazi yao na kuondokana na makazi holela
“Tunaomba wananchi wa maeneo mengine wenye matatizo kama yetu watuunge mkono wafanye kama tulivyofanya sisi kwani watapata maisha bora kwani thamani ya ardhi yao itapanda na kuwa na thamani kubwa”alisema
Alieleza zaidi kuwa huduma za jamii kama maji ya bomba,umeme,barabara na miundombinu mingine itawafikia kama ambavyo wananchi wa kata ya Mshangano wanavyotegemea kupata mara baada ya mradi kukamilika
Kibiki alisema kuwa katika mradi huo wananchi watapata faida nyingi ikiwemo ya ajira kuanzia hatua ya kupima viwanja kwani mchoro mmoja umetoa ajira kwa watu 40 ambao wamekuwa wanalipwa  Tshs 4000/= kwa kutwa moja na kwamba kwa michoro 23 itatoa ajira kwa watu 920
Alifafanua kuwa kwenye uchongaji wa barabara mchoro mmoja umetoa ajira kwa watu 80 ambapo kila mmoja analipwa Tshs 5000/= kwa kutwa hivyo michoro 23 itatoa ajira kwa watu 1840 ambapo jumla ya michoro yote 23 wananchi watakao kuwa wamepata ajira kwenye upimaji na kuchonga barabara ni watu 2760 wanawake na wanaume
Alieleza jumla ya fedha watakayokuwa wanapata wananchi wa kata hiyo kwenye upimaji wa viwanja ni 920X4000=3680,000/= na kwenye uchongaji wa barabara 1840x5000=9,200,000/= na kufanya jumla ya fedha yote kuwa ni Tshs 12,880,000/= kwa siku
Alifafanua kuwa wafanyakazi hao watatoka ndani ya kata ya Mshangano ambapo mradi unatekelezwa kwani hiyo inaweza kuwasaidia sana wananchi kujikimu kimaisha na kumudu kununua pembejeo za kilimo katika msimu huu na hivyo kuzalisha mazao kwa wingi
Naye  Diwani wa Kata ya Mshangano Faustine Mhagama akizungumza kwenye uzinduzi huo alisema kuwa mti wenye matunda ndio unaopigwa mawe hivyo kwa kuwa mradi huo una manufaa kwa wananchi wake umekuwa ukipigwa sana mawe,lakini hata hivyo anasema atasimamaimara kupigania haki za wananchi wake.
Anasema kuwa  kwa mradi huo wananchi wamenufaika kwa kuweza  kuuza viwanja vyao kwa bei kubwa lakini pia Halmashauri imepunguziwa gharama  ya kulipa fidia ambayo mara nyingi imekuwa ikichelewa kulipa au kushindwa kulipa na kuzua malalamiko na migogoro kwa wananchi
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya Ardhi Plan inayopima viwanja hivyo Gombo Samandito anasema kuwa Mradi huo ni wa  aina yake hapa Nchini na kwamba hakujawahi kuwa na mradi kama ule wa kupima viwanja 18,000 kwa muda mfupi tangu nchi ipate uhuru na kwamba dhamira yao ni kuona wananchi wakiishi katika makazi bora.
Samandito alisema kuwa mradi huo umeisaidia sana Serikali  kwani umeipunguza tatizo la kushindwa kupanga mji kutokana na ukosefu wa fedha za kugharamia mipango stahiki ya makazi bora kwani wananchi wa Mshangano wamethubutu kupanga mji kwa gharama zao jambo ambalo halijawahi kutokea kwa wananchi kupima viwanja vingi kiasi hicho kwa gharama zao
Mwandishi wa Makala
Anapatikana Simu 0755-335051/0715-335051/0784-335051/0778-335051
Barua pepe;stephano12mango@yahoo.com

No comments:

Post a Comment