About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, November 5, 2011

VETA RUVUMA KUWAFUATA WAHITAJI MAFUNZO KWENYE MAENEO YAO

Mkurugenzi wa VETA kanda ya Kusini Monika Mbelle

Na Gideon Mwakanosya,Songea
MAMLAKA ya mafunzo ya ufundi stadi(VETA) Mkoani Ruvuma imeanza kutoa mafunzo ya ufundi wa aina mbalimbali na udereva maeneo ya vijijini kwa malengo ya kupunguza ajali na kuwafuata wahitaji huko waliko na kukuza uchumi wa wananchi wa vijijini kupitia ufundi.
 
Mku wa Chuo hicho Mkoani humo  Gideon Ole Lairumbe akizungumza na mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com ofisini kwake jana amesema mafunzo hayo kwa kuanzia yamefanyika katika  kijiji cha Langiro Wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma ambapo  wananchi 45 wamenufaika na mafunzo hayo ya wiki mbili huku wengine 56 wakijiandikisha kwa mafunzo mengine.
 
Alisema kuwa baada ya mafunzo hayo kwenye kijiji hicho mafunzo mengine yatafuata kwenye kijiji cha Luanda ,Liuli na Mbamba’bay katika Mji mdogo wa Mbamba bay Wilayani humo.

Lairumbe alisema mafunzo yaliyotolewa ni ya ufundi wa umeme jua ili waweze kunufaika  na nishati hiyo vijijini,ufundi wa kutengeneza pikipiki na udereva wa pikipiki na magari na kwamba kwa kuanzia wametoa mafunzo ya ufundi na udereva wa pikipiki kwa wiki mbili katika kijiji cha Langilo.
 
‘Tumejipanga kutoa mafunzo haya kwa lengo la kuwanufaisha wananchi hivyo natoa wito kwa WanaRuvuma  kuunda vikundi na kuomba mafunzo ili tuwaletee mafunzo hukohuko vijijini’alisema Mkuu huyo wa Chuo cha Veta Ruvuma .
 
Alisema kuwa mafunzo ya udereva wa magari na pikipiki yanatimiza maagizo ya Serikali ya kuwa na madereva wenye sifa wanaofuata sheria za barabarani hivyo kuamua kubadili leseni za madereva wote na kuzifanya ziwe za kisasa zaidi.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Nyanda za juu kusini inayojumisha Mkoa ya Mbeya,Iringa na Ruvuma , Monica Mbelle alsema kuwa baada ya Serikali kuruhusu pikipiki kutumika kama chombo cha kubebea abiria jamii imeshuhudia  ongezeko kubwa la ajali za barabarani.
 
Alisema kuwa  Wilaya ya Mbinga ina pikipiki nyingi kuliko Wilaya nyingine Mkoani Ruvuma na kwamba wenye pikipiki hizo wako mjini na vijini na kwa sababu hiyo anasema VETA ikaamua kuwafuata wahitaji wa mafunzo ya udereva huko waliko ili waweze kupata mafunzo hayo huku wakiendelea na   shughuli nyingine.
 
Akifunga mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya  Mbinga Kanali Mstaafu  Edmund Mjengwa aliwataka wahitimu wa mafunzo hayo kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kupunguza wimbi la ajali.
 
‘Mtambue kwamba ujuzi mlioupata hautakuwa na maana kama hamtautumia kwa manufaa yenu na kwa jamii inayowazunguka na katika hili mwendesha pikipiki asipoendesha kwa kufuata shera za usalama barabarani atapoteza maisha yake na ya abiria wake na  hii itakuwa haina maana kwa mafunzo haya’alisema.
 
Aliwataka madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani na kwamba wasipozingatia sheria za usalama barabarani na kusababisha ajali watachukuliwa hatua kali za kisheria.
MWISHO

No comments:

Post a Comment