About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, November 5, 2011

UHABA WA SARUJI RUVUMA KUTOKUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI

                           Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu
 Na Mwandishi Wetu,Songea
IMEBAINIKA kupanda kwa bei ya saruji Mkoani Ruvuma kutoka kati ya sh. 15000 na sh. 18,0000 na kufikia sh. 20000 hadi 25,000 kwa mfuko mmoja wa kilo 50 kumetokana na saruji hiyo inayozalishwa Mkoani Mbeya kuuzwa nje ya ya nchi na nyingine chache kuuzwa kwenye Makampuni makubwa yanayotengeneza barabara Mkoani Ruvuma,
 
Uchunguzi uliofanywa na www.stephanomango.blogspot.com  kwa kuzungumza na Mawakala wa kuuza saruji umebaini kuwa saruji hiyo nyingi imekuwa ikiishia nje ya nchi hasa Malawi na hivyo Mkoa wa Ruvuma hupata mgao mdogo unaoishia kwenye makampuni makubwa ya kutengeneza barabara.
 
Gazeti hili lililotembelea kwenye maduka ya kuuza saruji lilishuhudia kuadimika kwa bidhaa hiyo na kubaki maduka matatu pekee yakiuza kwa bei ya juu huku baadhi ya mawakala wakidai wanaiuza bidhaa hiyo kwa bei ya juu kwa kuwa wanainunulia kwenye soko la Makambako na si Mbeya ambako inatengenezwa.
 
Mmoja wa Wafanyabiashara ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini alisema wamekuwa wakisafirisha saruji toka Makambako kwa bei ya sh. 2000 kwa mfuko,bei inayodaiwa kuwa ni kubwa sana na kwamba kama ingesafirishwa na kampuni ingesafirishwa kwa bei ya chini hivyo saruji ingeuzwa kwa bei ya awali. 
 
Kupanda kwa bei ya mfuko wa Saruji kumewapa wakati mgumu wakandarasi  mkoani Ruvuma  katika  kutekeleza miradi ya ujenzi inayofanywa na baadhi yao na kuhofia miradi hiyo kutotekelezeka kwa wakati kama mikataba yao inavyo wataka .
 
Wakiongea na mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com
  kwa nyakati tofauti wakandarasi hao walisema kuwa miradi mingi ambayo inajengwa hivi sasa haitamalizika kwa wakati kutokana na mfumuko wa bei ya vifaa vya ujenzi ikiwamo saruji kuwa kubwa na kuwafanya kushindwa kumudu gharama za ununuzi wa vifaa hivyo .
 
Mmoja wa wakandarasi hao Victor Ngongi alisema kuwa bei walizo andikia pindi wanaomba miradi hiyo zimekuwa tofauti na ilivyo sasa ambapo awali mfuko mmoja wa saruji uliunzwa kwa bei ya shilingi 15,000 hadi 18,000 jambo ambalo kwa sasa mfuko mmoja unauzwa kwa bei ya shilingi 20,000 hadi 25,000.
 
Ngongi alisema kufuatia hali hiyo baadhi ya  wakandarasi hao wameonyesha nia ya kuiandikia Serikali barua ya kusimamisha kuendelea na shughuli ya miradi ya ujenzi huo kwa lengo la kuepusha gharama zisizo kuwa za lazima kulingana na mikataba  waliyokubaliana ikiwemo kukabidhi kazi kwa wakati.
 
Hata hivyo baadhi ya wakazi wanaoishi mkoani humo walipohojiwa walisema kuwa suala hilo la mfumuko wa bei ya vifaa vya ujenzi  Serikali isipochukua hatua za haraka katika kudhibiti mfumuko huo  kunaweza kuahatarisha  majengo mengi kujengwa chini ya kiwango jambo ambalo ni hasara kwa serikali.
 
Naye wakala wa uuzaji wa saruji kupitia kampuni ya Mohamed Enterprises  Mkoani Ruvuma   Sadick Yusuph [Mpemba] alisema kuwa kuadimika kwa saruji hiyo kunatokana na saruji nyingi kuuzwa nje ya nchi na  asilimia kubwa ya mgao  huchukuliwa na makapuni makubwa ambayo yanajishughulisha na ujenzi wa barabara jambo  linalofanya asilimia inayobaki kuwa ndogo na kushindwa kutosheleza mahitaji.

Makampuni makubwa yanayojenga barabara Mkoani Ruvuma ni Sinno Hydro inayotengeneza barabara ya kutoka Peramiho hadi Mbinga,Sogea Sotom inayotengeneza barabara ya Songea hadi Namtumbo na Progresive inayotengeneza barabara ya Namtumbo hadi Tunduru ambazo zote zinatengenezwa kwa kiwango cha lami.

Aidha Sadick alisema kuwa njia pekee ya   kukabiliana na changamoto hiyo katika kufanikisha kupungua kwa bei  ni vyema viwanda vinavyotengeneza bidhaa hiyo vikaongeza uzalishaji zaidi kwa lengo la kutosheleza mahitaji ya wananchi .
 
Kwa upande wake Katibu Tawala wa mkoa wa Ruvuma Dr. Anselm Tarimo amewaagiza wafanya biashara wa saruji Mkoani humo kuangalia uwezekano wakupunguza bei ya bidhaa hiyo ambayo imepanda ghafla na kuwaumiza wananchi.
 
Alisema kupanda huko kwa saruji kunatokana na mgomo baridi kunatokana na mgomo baridi wa Wasafirishaji wanaosafirisha saruji kutoka Mbeya kuleta Songea wakati ambao wanaitoa Makambako wakati ambako ilitakiwa kusafirishwa na kampuni ya Tembo sementi ya Mbeya na kwamba  Makambako kuna saruji ya kutosha.
 
Alisema mfumo wa usafirishaji ndio unaoyumbisha bei hivyo Mkoa unajipanga kukutana na wasafirishaji na kuzungumza nao ili kuweza kutatua tatizo hilo ambalo linakwamisha miradi ya ujenzi ya maendeleo. 
 MWISHO.

No comments:

Post a Comment