About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, November 4, 2011

WAZAZI WAUNGANA NA WATOTO WAO KUMKATAA KAIMU WA KAIMU WA MKUU WA SHULE

Naibu wa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Phillip Mulugo

Na Augustino Chindiye,Tunduru

WAZAZI wa Wanafunzi wanaosoma katika Shule ya Sekondari ya Mataka Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma wameungana na Watoto wao kumkataa kaimu Mkuu wa Shule hiyo Mwl. Steven Makina aliyeombewa kukaimu nafasi hiyo baada ya kuhamishwa aliyekuwa Mkuu wa Shule hiyo Mwl Johnes Liombo.

Hayo yalijitokeza katika kikao cha dharula kati ya walimu,wazazi na viongozi wa Wilaya hiyo kilichofanyika katika viwanja vya shule hiyo  ambapo pamoja na mambo mengine wazazi hao wamekitafsiri kitendo cha kuletwa kwa kaimu Mkuu wa shule hiyo kuwa kinatokana na rushwa.

Sambamba na tukio hilo pia Baraza la wazee wa Wilaya ya Tunduru nao wametoa tamko na kuunda tume itayo onana na uongozi wa Wilaya hiyo zikiwa ni juhudi za kumtaka Mwl. Johnes Liombo arudishwe Shuleni hapo vinginevyo wataiomba Wizara ya Elimu iifutwe Shule hiyo wakidai kuwa wamechoka kuburuzwa na watu wanaojiita wazawa.

Wakiongea kwa nyakati tofauti Ally Buji, Hasan Kindamba, Akimu Mbuula na Daria Rashidi mbali na kudai kuchoshwa na tabia za viongozi wa Wilaya hiyo kupeleka Makaimu wakuu wa Shule kwa muda mrefu walisema kuwa hawapo tayari kusikia lolote juu ya mabadiliko hayo isipokuwa wao wanamtaka Mwl. Liombo arudishwe shuleni hapo.

Nao Alli Mponda , Matumla Sekula na Fadhili Makanjila katika maelezo yao wakapigilia msumali wa moto kuwa mbali na watumishi wazawa wa Wilaya hiyo kuhubiri ukabila na kutamani nafasi zote zishikwe na kabila la Wayao wenzao lakini kitendo hicho kina lengo la kuididimiza wilaya yao na kuongeza kuwa kuhamishwa kwa Mwl. Liombo ambaye siyo mzawa wa Wilaya hiyo kunaonesha kuwepo kwa ukabila katika Wilaya yao na ama kuna kitu kilichojificha nyuma yake.

Aidha wazazi na walezi hao pia walikejeli kauli iliyotolewa na kaimu Mkurugenzi wa Halmashuri hiyo Mwl Rashidi Mandoa kuwa Shule hiyo inaye Mkuu wa Shule ambaye ni Mwl Hasan Mussa aliyepo masomoni wakidai kuwa mtindo wa kuwekeana nafasi kama wanavyofanya viongozi hao unatakiwa kufanywa katika mashirika yasiyokuwa ya kiserikali na si kwa nafasi kama ilivyo hiyo Serikalini.

Walisema wameamua kuungana na madai ya watoto wao kutokana na kuamini kuwa Mwl. Liombo alikuwa muadilifu na alikuwa na uchungu wa kuiinua Shule hiyo kitaaluma na wakatahadharisha kuwa endapo uongozi wa Wilaya hiyo hautachukua hatua za haraka kumrejesha Mwalimu huyo kuna hatari ya kutokea kwa maafa makubwa katika shule hiyo.

Awali akisoma taarifa ya mahudhurio ya wanafunzi hao tangu mgomo huo uanze kaimu wa kaimu  mkuu wa Shule hiyo Mwl. Oden Masengo alidai kuwa tangu utokee mgomo huo mahudhurio ya wanafunzi wanaosoma katika Shule hiyo yamepungua na kufikia wanafunzi 170 tu kati ya wanafunzi 570 wanaosoma shuleni hapo hali inayotishia kushuka kwa taaluma kutokana na walimu kutoingia madarasani.

Akijibu malalamiko hayo kupitia maelezo yaliyosheheni data za kukidhiri kwa utoro na utovu wa nidhamu wa Wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo Afiasa elimu wa Shule za Sekondari ya Wilaya hiyo Mwl. Alli Mtamila aliahidi kuyawasilisha maono yao  kwa Mkurungezni Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kwa ajili ya kuyatafutia ufumbuzi.

Mwisho.     

No comments:

Post a Comment