About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, December 5, 2011

AKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUKUTWA NA MENO YA TEMBO

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda
Na Gideon Mwakanosya, Songea

JESHI la Polisi Mkoani Ruvuma linamshikiria Fundi magali wa Kampuni ya Sumry Mjini Songea Ally Makumba (42) Mkazi wa Bombambili Manispaa ya Songea akikabiliwa na tuhuma za kukutwa na Vipande 12 vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilo 2.23 ambayo thamani yake ni shilingi milioni 2 na 45 elfu mia tatu kumi na mbili kwenye buti la basi la Kampuni ya Sumry lilikuwa likijiandaa kwa safari ya kutoka Songea kwenda Jijini Da es Salaam.

Akizungumza na mtandao wa www.stephanomango.blogspot.com jana Ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda amesema kuwa tukio hilo lilitokea Novemba 29 mwaka huu majira ya saa 11 alfajiri huko kwenye Kituo Kikuu cha Mabasi cha Mjini Songea.

Kamuhanda amefafanua kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio askari Polisi ambao walikuwa doria kwenye eneo la Kituo Kikuu cha basi walipata taarifa toka kwa Raia mwema kuwa kwenye basi la Sumry linalotarajiwa kuondoka kwenda Jijini Dar es Salaam kuna mtu ameweka mzigo ambao uko ndani ya begi ambalo ndani yake kuna meno ya tembo.

Ameeleza zaidi kuwa baada ya Polisi hao kupata taarifa kutoka kwa raia wema walikwenda kwenye eneo ambako basi hilo limeegeshwa huku abiria wakijiandaa kuingia kwa safari ya kuelekea Jijini Dar es Salaam na kuanza kufanya ukaguzi ambapo baadae walifanikiwa kulikuta begi kwenye buti ambayo ndani yake kulikuwa kuna vipande 12 vya meno ya tembo yenye uzito wa kilo 2.23 na thamani yake ni Milioni 2.45312 .

Amesema kuwa baada ya kulibaini begi hilo  Polisi walianza kupeleleza kuwa mzigo huo  ulikuwa umewekwa na nani au abiria gani na badea walifanikiwa kumkamata fundi Magali wa Kampuni hiyo ambaye anadai kuwa alikuwa ameuweka mzigo huo muda mfupi tu kabla ya askari kukamata meno ya tembo kwenye basi hilo lente namba za usajili T777BVD ambalo lililazimishwa kwenda kwenye Kituo Kikuu cha Polisi kwaajili ya Upelelezi zaidi.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Kamuhanda Polisi inaendelea kufanya upelelezi zaidi wa kina ili kubaini tukio hili na kwamba utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani kujibu mashtaka yanayomkabili.

MWISHO

No comments:

Post a Comment