About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, January 21, 2012

APANDISHWA KIZIMBANI KWA KOSA LA KUMBAKA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA TATU

Na Gideon Mwakanosya,Songea

MTU mmoja mkazi wa mtaa wa Ruvuma katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu mkazi mkoani humo kwa
tuhuma ya kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha tatu.

Ilidaiwa Mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka Wakili wa Serikali Shaban Mwegole mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Jenifer Changani
kuwa mnamo kati ya Januari na Mei mwaka jana, mshtakiwa Sababu Iddi(18) ambaye ni mkazi wa mtaa huo alitenda kosa hilo.

Mwendesha mashtaka huyo aliendelea kudai kuwa mwanafunzi huyo anasoma shule ya sekondari Ruvuma ambapo mshtakiwa ameonekana kutenda kosa hilo huku akijua kwamba ni kosa kisheria kufanya mapenzi na mwanafunzi jambo ambalo lilisababisha kukatisha masomo.

Kadhalika wakati kesi hiyo ikiendelea mahakamani hapo Hakimu mkazi wa Mahakama ya mkoa wa Ruvuma Shangani alisema mshtakiwa ana kesi ya kujibu kutokana na shtaka linalomkabili na kwamba anapaswa kuleta utetezi wake mahakamani.

Hata hivyo kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 14 mwaka huu itakapoletwa mahakamani kwa ajili ya kuanza kusikiliza utetezi wa mshtakiwa na kwamba mshtakiwa amerudishwa mahabusu kutokana na kukosa
mdhamini.

MWISHO.

No comments:

Post a Comment