About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, January 21, 2012

VILABU MANISPAA YA SONGEA KUANZA KUCHUKUA FOMU USHIRIKI LIGI YA SANGA ONE

 Mwenyekiti wa SUFA Golden Sanga, Maarufu kwa jina la Sanga One
Diwani Mstaafu na Mdau wa Michezo Golden Sanga(Sanga One) akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ligi ambayo inatarajia kuanza hivi karibuni mjini hapa

Na Stephano Mango,Songea

CHAMA cha mpira wa miguu katika Manispaa ya Songea(SUFA) kimezitaka vilabu kujitokeza kuchukua fomu kwa ajili ya kushiriki  mashindano ya Sanga One Cup ambayo yamepangwa kufanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Sokoine katika Manispaa hiyo.
 
Akizungumza mjini hapa jana, Katibu msaidizi wa SUFA, Godfrey Mvula alisema kuwa mashindano hayo yatahusisha vilabu vyote ndani ya Manispaa hiyo ambavyo vina usajili wa kudumu kutoka kwa msajili wa vyama vya michezo nchini na vile visivyokuwa na usajili huo.
 
Mvula alisema mashindano hayo yatadhaminiwa na mmoja wa wadau wa soka na pia Mwenyekiti wa SUFA katika Manispaa hiyo, Golden Sanga  maarufu kwa jina la Sanga One  yenye lengo la kusaka vipaji vipya na kuviibua ili kuwafanya wachezaji hao kuwa tegemeo na hazina kwa Manispaa mkoa na Taifa kwa ujumla.
 
Alisema mashindano hayo yatakuwa chachu na mbinu ambayo itasaidia SUFA  kuwapata wachezaji wenye vipaji na wanaojituma wawapo uwanjani badala ya kuwatafuta kwa kuwateua kupitia  kwenye mashindano ya ligi ya wilaya au mkoa na kuishia kutafuta maslahi yao binafsi badala ya mpira uliomweka hapo.
 
 Alieleza kuwa bingwa wa mashindano hayo ataondoka na kitita cha fedha taslimu Sh. 200,000/=,  wa pili atazawadiwa fedha Sh. 100,000/= na  mshindi wa tatu ataambulia fedha Sh.70,000/=, mchezaji bora atazawadiwa fedha taaslim Sh.20,000/= na timu itakayoonyesha nidhamu ya ndani na nje ya uwanja watapata fedha Sh.20,000/=.
 
Alisema gharama ya uchukuaji wa fomu imepangwa kulipia  Sh.10,000/= ambayo itapenda kushiriki mashindano hayo na zitarejeshwa fomu hizo Januari 26 mwaka huu saa 10:30 jioni kwenye ofisi za SUFA alidai mchezaji atakaye bainika amesajiliwa na timu zaidi ya moja jina lake litaondolewa kushiriki mashindano hayo.
 
MWISHO

No comments:

Post a Comment