About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, May 11, 2012

WAANDISHI WAASWA KURIPOTI KIKAMILIFU ADHA YA UMEME MANISPAA YA SONGEA

                            
MAHINDI YAKIWA KWENYE KIWANDA CHA MTAZAMO KWA AJIRI YA KUSUBIRI UMEME ILI YAKOBOLEWE NA YASAGWE 




Na Stephano Mango, Songea
WAANDISHI wa Habari mkoani Ruvuma wametakiwa kutumia taaluma yao kikamilifu katika kuwaokoa wananchi wanaoteseka kutoka na adha wanazozipata kutokana na mgawo mkubwa wa umeme usiokuwa na kikomo unaoendelea kuwakabili katika Halmashauri ya Manspaa ya Songea
Wito huo umetolewa jana na Mkurugenzi wa kampuni ya Mtazamo Enterpress, Julius Mlawa wakati akizungumza na waandishi wa habari jana waliotembelea kiwanda cha kampuni hiyo kinachojishughulisha na ukoboaji nafaka, usagaji na uuzaji wa unga
Mlawa alisema kuwa waandishi wa habari ndio jukwaa la wananchi wanyonge ambao sauti zao hazisikiki vizuri kusemea licha ya kuendelea kuteseka na adha ya mgao mkubwa wa umeme unaowasababishia kupanda kwa gharama za maisha
Alisema kuwa mashine za kusaga nafaka ambazo zipo katika baadhi ya maeneo ya Manispaa hiyo zimeshindwa kutoa huduma kwa muda muafaka na kusababisha wananchi walio wengi kulazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma nje ya Manispaa ambako kuna mashine za kusaga nafaka zinazotumia mafuta ya Dizeli na kusababisha bei ya huduma hiyo kupanda mara mbili ikilinganishwa na awali
Alieleza kuwa kitendo cha shirika la umeme mkoani humu kushindwa kutoa huduma hiyo kwa wakati mbali ya kusababisha usumbufu kwao lakini kimekuwa kikiwakosesha mapato ambayo wanayatumia kulipa kodi kwenye mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) kutokana na hasara zinazosababishwa na ukosefu wa umeme
Alifafanua zaidi katika kiwanda chake kuna wafanyakazi zaidi 30 ambao wanashinda kiwanda wakisubiri umeme ili waweze kufanya kazi bila mafanikio huku wakilipwa posho zao za kila siku bila kufanya kazi jambo linalosababisha hasara kubwa
Alieleza zaidi kuwa kutokana na ukosefu wa umeme ambao umekithiri katika manispaa ya Songea wafanyabiashara wengi wanashindwa kurejesha mikopo waliyokopa kwenye taasisi za fedha jambo ambalo ni hatari kwa biashara zao na jamii ambayo inanufaika na biashara hizo
Alisema kuwa kutokana na hali hiyo huenda akalazimika kusitisha kwa muda kutoa huduma ya usagaji na ukoboaji wa nafaka kama hali hiyo ya ukosefu wa umeme wa uhakika haitafanyiwa kazi na shirika hilo la umeme mkoani humu kwa sababu mbali ya kukosa mapato lakini imekuwa ni usumbufu kwa wananchi ambao wanahitaji huduma hiyo.
Kwa upande wake Meneja wa shirika la umeme mkoa wa Ruvuma Mhandisi Monika Kebara alikiri kuwepo kwa tatizo hilo na alisema hivi sasa huduma hiyo ya umeme inatolewa kwa mgawo kwa sababu uwezo wa ufuaji wa umeme umepungua sana kutokana na kuharibika kwa mitambo ya kuzalisha umeme iliyopo Kibulang’oma mjini hapa.
Kebara alisema kituo hicho kina mashine saba za kuzalisha umeme lakini kwa hivi sasa ni mashine tatu ndizo zinazofanya kazi hiyo kwa kutoa Megawati 2.6 wakati mahitaji ni Megawati 5 hasa ikizingatiwa kuwa katika mji wa Songea shirika hilo lina wateja elfu kumi na mbili.
Alisema kuwa tayari jopo la mafundi kutoka Jijini Dar es Salaam limefika kwa ajiri ya ukarabati mkubwa wa mitambo hiyo na kwamba mwishoni mwa mwezi mei kutakuwa na umeme wa uhakika
MWISHO

No comments:

Post a Comment