About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, July 24, 2012

MWANAFUNZI AFA MAJI KATIKA LAMBO LA KUNYWESHEA NG’OMBE

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki
Na Steven Augustino, Tunduru
MWANAFUNZI wa Darasa la nne katika Shule ya Msingi Majimaji Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma aliyefahamika kwa jina la Rehema Salum (12) amefariki dunia baada ya kutumbukia katika lambo la kunyweshea ng’ombe.

Mashuhuda wa tukio hilo wamedai kuwa marehemu alikubwa na mkasa huo wakati akijaribu kuogelea katika lambo hilo lililochimbwa na Idara ya magereza kwa ajili ya kunywesha Ng,ombe wa Gereza la Mifungo la Kilimo la Majimaji lililopo kijijini hapo.

Wakifafanua taarifa hiyo mashuhuda hao walidai kuwa katika tukio hilo marehemu alikuwa ameongozana na kundi la watoto wenzake kwa nia ya kwenda kuoga katika lambo hilo kama ambavyo hufanya siku zote na kwamba kilichotokea ni bahati mbaya iliyotokana na yeye kuogelea eneo
lenye kina kirefu.

Mganga aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu Rehema, Dkt. Mosses Mwahasunga alidai kuwa chanzo cha kifo hicho ni kukosa hewa kulikosababishwa na kunywa maji mengi.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki mbali na kukiri kuwepo kwake alidai kuwa polisi wanaendelea na uchuinguzi tukio hilo.
Mwisho

No comments:

Post a Comment