About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, January 19, 2015

DKT NCHIMBI; WANACCM WAJIPANGA SHEREHE ZA MIAKA 38 YA CCM TAIFA



MWENYEKITI WA KAMATI YA MAANDALIZI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 38 YA CCM TAIFA DKT EMMANUEL NCHIMBI AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI SONGEA

NA, STEPHANO MANGO, SONGEA

WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi Mkoani Ruvuma Wametakiwa kuendelea kujipanga Kikamilifu Katika Sherehe za Maadhimisho ya kutimiza miaka 38 ya kuzaliwa kwake ambayo yanatarajiwa kufanyika Katika Viwanja vya Majimaji Mjini Songea Februari 2 mwaka huu

Akizungumza na Waandishi wa Habari Jana katika Viwanja vya Ccm Mkoa wa Ruvuma Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Sherehe hizo za Maadhimisho ya miaka 38 Ccm Dkt Emmanuel Nchimbi alisema kuwa Maadhimisho hayo ni Muhimu sana kwani yanalenga zaidi kukumbuka toka kuzaliwa kwake hadi hapa kilipo hivyo wanaccm hawana budi kuhakikisha wanajipanga vizuri kufanikisha maadhimisho hayo

Dkt Nchimbi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo La Songea Mjini alisema kuwa Wanaccm wanatakiwa kutumia fursa hiyo muhimu kujiimarisha kiuchumi na kiutalii kwani kuwepo kwa wageni wengi wakati wa Maadhimisho hayo kutachangia ununuzi wa bidhaa mbalimbali ambazo zinazalishwa na Wajasiliamali Mjini hapa

Alisema kuwa Kitendo cha Viongozi Wakubwa  wa Ccm Taifa katika Vikao Vyao kuridhia kuwa Maadhimisho hayo Kufanyika Songea ni cha Busara sana hivyo Tunawajibika kujiandaa vyema kuwapokea Wageni na kufanya mambo ambayo yanaendana na maudhui ya Maadhimisho hayo

Alieleza kuwa Mwaka huu ni Mwaka wa Uchaguzi ni lazima wanachama na wapenzi wa chama hicho kuelezea mafanikio yaliyopatika katika miaka 38 ya kuzaliwa kwa chama hicho makini na kikubwa cha siasa nchini ambacho kinaongoza nchi kwa zaidi ya miaka 50 sasa

Alifafanua kuwa  Mafanikio ambayo chama hicho na kwa namana inavyotatua changamoto za Wananchi wake ndio msingi wa Vyama vya Upinzani Nchini kukionea  wivu na hata kukieneza vibaya katika mikutano yao ya hadhara

Hata hivyo amewataka Viongozi wote wa Jumuiya za Chama hicho kuendelea kujipanga ili kufanikisha Maadhimisho hayo  Muhimu yatahudhuriwa na wageni mbalimbali toka nchi jirani pamoja na wegeni kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini.
 MWISHO

No comments:

Post a Comment