About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, January 19, 2015

WAPIGA KURA NAMTUMBO WATAKIWA KUMFANYIA TATHIMINI MBUNGE WAO




                                             MBUNGE WA JIMBO LA NAMTUMBO VITA KAWAWA

NA, STEPHANO MANGO,NAMTUMBO

WAPIGA KURA  wa Jimbo La Namtumbo Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma Wametakiwa Kumfanyia Tathimini Mbunge wao  Vita Kawawa Waliomchagua  katika vipindi viwili Mfululizo Mwaka 2005 na Mwaka 2010 kama ametekeleza vyema Ilani ya Chama chake na Ahadi alizozitoa wakati anaomba kura katika Chaguzi mbili hizo

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mjini hapa Jana Afisa Elimu Mstaafu na Mfanyabiashara Ally Mbawala Alisema kuwa Mwaka huu ni Mwaka wa Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani hivyo ni fursa Muhimu Sana kwa Wananchi kuchukua tafakari Stahiki ya utendaji Kazi wa Wawakilishi wao waliowachagua vipindi vilivyopita na Kuwahukumu katika sanduku la kura

Mbawala Alisema Kuwa Kipindi hiki sio cha kufanya mchezo ni kipindi cha kujitendea haki kwa Kuangalia utatuzi wa Changamoto zilizokuwepo kabla ya kumchagua Kiongozi husika hadi leo ili kujiridhisha utendaji kazi wake na kama anataka kugombea tena basi ahukumiwe kwa mujibu wa kipimo chake cha utendaji Kazi

Alisema kuwa Jimbo la Namtumbo lina Fursa Nyingi  sana za Kimaendeleo kwani kuna ardhi nzuri, Misitu, Madini , Mbuga za Wanyama na Maliasili zingine nyingi na wananchi wake ni wakulima wazuri wa mazao mbalimbali ya chakula , hivyo ni muhimu kupima kama rasilimali hizo zimeweza kusimamiwa na kutumika vizuri na kama zimewezesha kuinua maisha ya wakazi wa Jimbo hilo

Alieleza Kuwa Jimbo hilo ndilo ambalo lilikuwa Maarufu kwa Kilimo Cha Tumbaku na Mbunge wa Jimbo hilo alikuwa ni Mwenyekiti wa Bodi ya Tumbaku Tanzania hivyo ni vyema  tukamtafakari kwa kina kama  ameweza kushiriki kikamilifu kufufua vyama vya Ushirika na kukuza zao hilo ambalo ndilo zao kubwa la kiuchumi kwa Wakazi wa Namtumbo

Alifafanua kuwa kabla ya uchaguzi ni muhimu sana Wapiga Kura wa Jimbo hilo wakawa na vipaumbele vyao vya Kimaendeleo ili waweze kutengeneza ajenda ya pamoja badala ya kusubiri ilani za Vyama au matakwa ya Mbunge ambayo kimsingi hayana tija katika maisha yao

“Mimi ni Mzaliwa wa Namtumbo lakini kila Siku Maisha ya Wakazi Wa Jimbo hili yanazidi kuwa magumu kwa sababu mbalimbali hali ambayo ina hatarisha amani na utulivu katika jamii kwani kundi la walionacho wanaendelea kunufaika huku kundi kubwa la wasio nacho wakiendelea kuhangaika”

Alieleza zaidi kuwa  hadi leo bado kuna Wakazi wa Jimbo hilo hawajafikiwa na huduma za Maji Safi Na Salama, Elimu,  Afya, Miundombinu, huduma za kiuchumi na Mawasiliano hali ambayo inaendelea kuwafanya wawe masikini zaidi
MWISHO



No comments:

Post a Comment