About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, August 30, 2011

KAIMU MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA ANNA MBOGO

                                  

                                         WANANCHI SONGEA WAIFYATUKIA WIZARA YA AFYA
                                     Na Stephano Mango,Songea
 
WANANCHI wa Vijiji vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma wameiomba Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuona umuhimu wa kuwaletea watumishi wenye taaluma wakiwemo wauguzi na Waganga kwenye Zahanati na vituo vya Afya ambako kuna Upungufu wa Wataalamu.
 
Wakizungumza kwa Nyakati tofauti na mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ wananchi hao wameeleza kuwa kwenye baadhi ya Zahanati na Vituo vya Afya vilivyopo Wilayani Songea kuna tatizo kubwa la upungufu wa Wauguzi na Waganga ambao umekuwa ukisababisha kuwepo kero kubwa kwa Wakazi wa Vijiji hivyo.
 
Hebron Mbilinyi Mkazi wa Kijiji cha Madaba alisema kuwa katika Kituo cha Afya cha Madaba kina wauguzi na waganga wachache na kusababisha kuwepo msongamano mkubwa wa wagonjwa wanaofika kupata tiba kwenye Kituo hicho.
 
Alisema kuwa huduma inayotolewa kwenye Kituo hicho cha Afya ni duni kwani wakati mwingine wagonjwa ambao wana uwezo kifedha hulazimika kutafuta Hospitali za kulipia ambako hupatiwa matibabu.
 
Said Hussein Mkazi wa Kijiji cha Muhukuru alisema kuwa Kituo cha Afya cha Muhukuru kimekuwa na tatizo kubwa la kutokuwa na Waganga hasa ikizingatia kuwa kina Mganga mmoja tu ambaye hulazimika kutoa huduma tangu asubuhi na wauguzi waliopo ni wachache hivyo anaiomba Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ione umuhimu wa kuwakumbuka wakazi wa Muhukuru kwa kuwapelekea Wataalamu wenye sifa ambazo zitapunguza kero zilizopo Kijijini hapo ambako kuna umbali wa Kilomita 80 tokea Songea Mjini ambako kuna Hospitali ya Serikali ya Mkoa.
 
Fadhili Ngonyani Mkazi wa Kijiji cha Liyangweni alieleza zaidi kuwa Huduma inayotolewa katika Zahanati ya Kijiji hicho siyo ya kuridhisha kwasababu Zahanati hiyo ina Wauguzi wachache ambao ndiyo wamekuwa wakitoa huduma badala ya Mganga ambaye hajaletwa tangu muda mrefu hivyo ameitaka Halmashauri ya Wilaya hiyo kuchukua hatua za haraka kutafuta Waganga pamoja na Wauguzi kwenye Zahanati hiyo ili kupunguza kero iliyopo Kijijini hapo.
 
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Anna Mbogo aliuambia mtandao huu kuhusiana na kuwepo kwa malalamiko toka kwa Wananchi ya upungufu wa wataalamu kwenye Zahanati na Vituo vya Afya alikiri kuwa Halmashauri yake ina upungufu wa Wataalamu kwenye Zahanati na Vituo na Afya.
 
Mbogo alisema kuwa Halmashauri hiyo ina Vituo viwili vya Afya ambapo alivitaja kuwa ni Kituo cha Afya cha Muhukuru na Kituo cha Afya cha Madaba ambavyo vyote vina waganga watatu tu badala ya kuwa na waganga wanne kila kimoja.
 
Alifafanua kuwa Halmashauri hiyo pia ina Zahanati za Vijiji 23 ambazo zina wauguzi na waganga wachache na baadhi ya Zahanati zilizopo hazina waganga na badala yake wauguzi ndiyo wamekuwa wakitoa huduma kwenye Zahanati hizo.
 
Alizitaja Zahanati ambazo hazina kabisa waganga kuwa ni Liyangweni,Nambendo,Gumbiro na Ngahokola na Kituo cha Afya cha  Muhukuru kina mganga na Madaba kuna waganga wawili wakati kila Kituo cha Afya kulipaswa kuwe na waganga wanne na kwenye Zahanati kunapaswa kuwe na waganga wawili.
 
Alieleza zaidi kuwa kutokana na hali hiyo kwenye vituo vya afya kuna upungufu wa waganga watatu na kwenye Zahanati kuna upungufu wa waganga 29 wakati mahitaji ya waganga kwenye Halmashauri hiyo bado ni kubwa na kusababisha kuwepo Changamoto kubwa ya upungufu mkubwa wa wataalamu wenye sifa wakiwemo wauguzi na waganga  jitihada inaendelea kufanywa ya kutafuta waganga na wauguzi wenye sifa kujaza nafasi zenye upungufu kwenye Zahanati
 

No comments:

Post a Comment