About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, August 30, 2011

MIKARATUSI NI MITI HATARI KATIKA VYANZO VYA MAJI KWENYE MILIMA YA MATOGORO

                             Na Thomas Lipuka,Songea
 
IMEBAINI kuwa ukosefu wa maji kiangazi katika Manispaa ya Songea unachangiwa kwa kiasi kikubwa na aina ya miti ambayo ipo katika misitu ya milima Matogoro ambayo hunyonya maji kwa kiwango kikubwa kwa kipindi cha mwaka.
 
Afisa maliasili wa Mkoa Ruvuma Enock Buja akizungumza na mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ alisema utafiti uliofanywa na Taasisi inayoshughulikia utafiti wa misitu nchini ijulikanayo kama  TAFORMA, imebaini kuwa kuna aina kadhaa ya miti ambayo kwa kiwango kikubwa.
 
Ameitaja miti hiyo kuwa ni mikaratusi (Camaldulensis) ambayo hunyonya maji kiasi cha milimita 1240 kwa mwaka na mikaratusi aina ya (Microrhea) pia hunyonya maji milimita 1050 kwa mwaka.
 
Afisa maliasili huyo wa Mkoa amefafanua kuwa ,aina nyingine ya miti inayonyonya maji kwa wingi ni mikaratusi hujulikana kama patula wenye uwezo wa kunyonya maji kiasi cha milimita 665 kwa mwaka.
 
Katika ufafanuzi Buja amesema miti hiyo yote iliyo tajwa ipo misitu ya milima matogoro ambapo kiasi mingi imeondolewa kwa maji ikiwa kiasi, tu ikiwa na lengo la kuiondoa isilete hatari ya kukosekana kwa maji,kwa wakazi wa Manispaa ya Songea.
 
Afisa maliasili huyo ameongeza kusema kuwa kiasi kilichotajwa hunyonywa na miti hiyo ambapo  kwa mti mmoja na sio kwa uwingi wake katika misitu.
 
Katika utafiti huo imeelezwa kuwa ipo miti mingine kwa mfano mgunga na mvile inayoelekea kutumia maji mengi kuliko mikaratusi iliyotajwa hapo juu.
 
Amesema baadhi ya mazao ya kilimo mathalani mpunga na miwa nayo hutumia kwa kiwango ambacho karibu sawa ya mikaratusi.
 
Katika msukumo wa Kitaifa  wa kupunguza umaskini MKUKUTA mbinu nyingi zinafikiliwa kutumika katika kufikia azma hiyo bahati mbaya upandaji miti katika vyanzo vya maji haujatiliwa mkazo kwa umakini hasa miti gani ipandwe ili kuondokana na tatizo la miti kunyonya maji.
 
Ni sahihi kabisa kuvuna miti iliyopo misitu ya milima matogoro kwani miti hiyo ni hatari na ni adui mkubwa wa chanzo kikuu cha maji yatumiayo katika Manispaa ya Songea.
 
Hivi sasa Taifa limeagiza kuwa kila Wilaya ipande miti zaidi ya 1500 ili kurudisha jotoridi  na kuondoa hewa ya ukaa ambayo inatishia Taifa letu kwa tabia mbaya za baadhi ya watu wakatao miti bila kupanda au kwa ajili ya mkaa na shughuli za ujenzi na za kibinadamu.
 
Hali ya uchomaji moto ni tatizo la pili katika misitu ya milima matogoro mbali ya juhudi za mkoa za kurudishia miti hiyo mwaka hadi mwaka kwa utaratibu wa kupanda miti ya asili ambayo hainyonyi maji kwa wingi jambo hilo juhudi zake linafifishwa na watu waharibifu wanaoendeleza vitendo vya uchomaji moto katika mlima matogoro na misitu yake  Mkoani  Ruvuma.

No comments:

Post a Comment