About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, September 12, 2011

ASKARI WANYAPORI AKUTWA AMEUWA NA WATU WASIOFAHAMIKA

                                               Na Gideon Mwakanosya,Songea.
ASKARI wa idara  ya wanyamapori Nchini  Msumbiji  Babu Abdalah (35) amekutwa akiwa ameuwawa kwa kupigwa na kitu chenye ncha kali sehemu za kifuani na watu wasiofahamika huko katika  kijiji cha Chikomo wilayani Tunduru Mkoa wa Ruvuma.
Akizungumza na Mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ ofisini kwake jana kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda alisema kuwa tukio hilo limetokea Septemba 10 mwaka huu majira ya saa 9 alasiri huko katika kijiji cha Chikomo.
Alisema kuwa siku hiyo ya tukio inadaiwa kuwa afisa mtendaji  wa kijiji hicho Ally Mtukusye alipatiwa taarifa ya tukio hilo kasha aliwasiliana na polisi wa kituo kikuu cha Tunduru ambao walifika kwenye eneo la tukio wakiwa wameongozana na mganga ambaye ndiye aliyethibitisha kuwa askari huyo wa idara ya maliasili toka Nchi ya Msumbiji amekufa kutokana na kipigo.
Kamuhanda alisema kuwa  Askari huyo alikutwa akiwa na majeraha makubwa sehemu za usoni upande wa kushoto na kifuani upande wa kushoto ambayo  ndio yalimsababishia  kuvuja kwa damu nyingi atimaye kufariki dunia.
 Hata hivyo kamanda Kamuhanda alisema kuwa kufuatia tukio hilo hakuna aliyekamatwa au kutiliwa mashaka na chanzo bado kinaendelea kuchunguzwa.
MWISHO.

No comments:

Post a Comment