About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, September 12, 2011

MAELFU YA WAKAZI WA TUNDURU WAJITOKEZA KUMZIKA MWENYEKITI WA TLP TUNDURU RAJABU MNYACHI

                             Na  Steven  Auguastino, Tunduru
 
MAELFU ya wakazi wa mji wa Tunduru wamejitokeza kumzika aliyekuwa Mwenyekiti wa chama cha Tanzania Labour Party (TLP) Wilaya ya Tunduru Rajab Mohamed Mnyachi aliyefariki Dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu na kulazwa katika hospitali ya serikali ya wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma.
 
Msemaji wa familia ya Marehemu Mnyachi Bw. Shaibu Namkumbe akizungumza na mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ alisema kuwa marehemu Mnyachi alikuwa anasumbuliwa na  maradhi ya shinikizo la damu.
 
Akifafanua wasia wa marehemu mnyachi Bw. Namkumbe alisema kuwa kipindi cha uhai wake alijishikisha na alikuwa mkereketwa wa mageuzi kupitia vyama ya siasa pamoja na kugombea nyadhifa mbali mbali.
 
Alisema mwaka 1986 hadi 1999 marehemu  Mnyachi alikuwa mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi na aligombea katika kinyang`anyiro cha Ubunge wa jimbo la Tunduru akiwa anapambana na marehemu Juma jamardini Akukweti wa CCM katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995.
 
Taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa Mwaka 1999 marehemu alikihama chama cha NCCR Mageuzi na kujiunga na TLP ambako pia alichaguliwa kuwa mwenyekiti wake hadi umauti ulipo mkuta Septemba 9 mwaka huu.
 
Akiwa katika chama hicho pia marehemu alitoa hamasa kubwa na kukifanya chama hicho kupata wanachama wengi na kugombea katika vinyang`anyiro vya Ubunge katika chaguzi za mwaka 2000, 2005 na uchaguzi mdogo wa kuziba pengo la marehemu Akukweti mwaka 2007.
 
Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi wanaomfahamu Marehemu Mnyachi, katibu wa Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini Bw. Maulidi Kalambo (Yakanungu) na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Wilaya ya Tunduru Bw. Maurid Said mbali na kukiri kuwa Marehemu alikuwa mahiri katika medani za siasa na kuongeza kuwa sasa Tunduru imeishiwa watu wenye vipaji.
 
Katika maelezo yao viongozi hao walisema kuwa Marehemu mnyachi, marehemu  Mazee Rajab wa CUF pamoja na Simbili Makanyaga wa UDP aliyehamia jijini Dar es salaam baada ya kuchaguliwa kuwa katibu Mwenezi wa Chama hicho Taifa walikuwa ni hazina kubwa na kwamba sasa Wilaya ya Tunduru inategemea majaliwa ya mungu kupata vijana wenye kipaji na watakao kubalika katika kuleta changamoto za maendeleo vinginevyo CCM itaendelea kushika hatamu.
 
Mwisho.   

No comments:

Post a Comment