About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, September 12, 2011

NIMESAFIRI KIKAZI WAPENZI WASOMAJI WA MTANDAO HUU

Stephano Mango
Mmiliki wa mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/, ambaye ni ndugu Stephano Mango amesafiri kikazi toka Songea mpaka Jijini Dar Es Salaam, ambapo ameungana na wanaharakati wengine nchini na nchi jilani kwa ajili ya kuhudhuria Tamasha la Jinsia Tanzania ambalo linaanza kufanyika kesho Septemba 13-16 mwaka huu 2011

Katika Tamasha hilo Mada mbalimbali zitawasilishwa na wanaharakati na wasomi waliobobea katika utetezi wa masuala ya jinsia na haki za binadam, kwa mwaka huu Mada itakuwa ni ,"Ardhi,Nguvu Kazi na Maisha Endelevu" chini ya Kampeni kubwa ya "Haki ya Uchumi:Rasilimali ziwanufaishe Wanawake Walioko Pembezoni.

Hivyo,ndugu wasomaji jiandaeni kupata habari mbalimbali kutoka katika tamasha hilo kwani mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com,utakuwa/ makini kuwaletea wasomaji vitu murua kwa kukidhi kiu yako ya kupata matukio muhimu ya kiharakati

No comments:

Post a Comment